Na Bertha Lumala, Dar es Salaam
          Kiungo mkongwe wa simba SC Amri Kiemba leo asubuhi ameibuka          katika mazoezi ya Azam FC yaliyoanza baada ya mapumziko ya wiki          mbili kujiandaa kwa mechi ya raundi ya nane ya Ligi Kuu ya          Vodacom Tanzania Bara (VPL) dhidi ya Yanga SC itakayochezwa          kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Desemba 28, mwaka          huu.
          Kuibuka mazoezini kwa Kiemba kunakuja ikiwa ni siku mbili tu          baada ya Simba SC kutangaza kupitia kwa msemaji wake Hamphrey          Nyasio kumpeleka Aza FC kwa mkopo kiungo huyo aliyekuwa          amesimamisha kwa madai ya utovu wa nidhamu na kucheza chini ya          kiwango awamo klabuni msimbazi.
          Kiemba, kiungo mpya wa Simba SC, Shaban Kisiga na winga Haroun          Chanongo walisimamishwa na uongozi wa klabu hiyo muda mfupi          baada ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Tanzania Prisons kwenye          Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya Oktoba 25, mwaka huu          na kumriwa kurejea jijini Dar es Salaam kwa mahojiano zaidi.
          Kisiga alisamehewa baada ya kukiri makosa na kuomba radhi lakini          Kiemba na Chanongo walibaki kwenye hali ya 'moshi mweusi.'
          Azam FC walipeleka dili ya kumtaka kwa mkopo kiungo huyo          anayefanya vizuri akiwa na Taifa Stars lakini Simba SC walikataa          ofa hiyo wakitaka Azam FC imnunue moja kwa moja badala ya          kumtaka kwa mkopo vingine wapewe beki Said Morad ambaye ni wazi          hatakuwa na namba katika kikosi cha kwanza cha Mcaeroon Joseph          Omog baada ya kusajiliwa kwa beki kisiki Serge Wawa kutoka          El-Marreikh ya Ligi Kuu ya Sudan.
Comments
Post a Comment