
Na                  Mwandishi wetu,Mara.
        KIKUNDI cha Wanaume                 wapiga kasia cha JJ Buda kutoka Nyarusurya Mkoani Mara                kimeibuka na ubingwa katika fainali za Mkoa za mashindano                yambio za mitumbwi chini ya udhamini wa bia ya  Balimi                Extra Lager zijulikazo kama "Balimi Boat Race 2014" na                hivyo kikundi hicho kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi                900,000/= pamoja na kuwakilisha Mkoa wa Kagera kwenye                fainali za Kanda zinazotarajiwa kufanyika Desemba 6 mwaka                huu jijini Mwanza.
        Nafasi ya pili                ilichukuliwa na kikundi cha Benedict Chamba ambacho                kilizawadiwa pesa taslimu Shilingi 600,000/= pamoja na                kuwakilisha mkoa katika fainali za Kanda jijini Mwanza                pia, wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha                Tumaini Maendeka kutoka Kisorya ambacho kilizawadiwa pesa                taslimu Shilingi 500,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa                na kikundi cha Bernard Charles kutoka Nyarusurya ambacho                kilizawadiwa Shilingi 400,000/=
        
Nafasi                  ya tano hadi ya tisa walipewa kifuta jasho cha pesa                  taslimu Shilingi 250,000/= kila kikundi ambavyo ni Siagi                  Siagikutoka Kinesi, Chuma Musa kutoka Kinesi, Matiku                  Nkoba kutoka Kuruya, Paul Mwita kutoka Nyarusurya,                  Ostadhi Magori Kutoka Kuruya na Emmanue Jemes kutoka                  Resti
        Upande wa Wanawake                kikundi cha Nyamizi Deokutoka Kisorya kilifanikiwa kutwaa                ubingwa na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu Shilingi                700,000/= pamoja na nafasi ya kuwakilisha mkoa katika                fainali za Kanda jijini Mwanza. 
        Nafasi ya pili Wanawake                ilichukuliwa na kikundi cha Maria Sarige ambao                walizawadiwa Shilingi 600,000/=,washindi wa tatu ni                kikundi cha Edina Peterkutoka Bwai ambao walizawadiwa                Shilingi 400,000/= na nafasi ya nne ilichukuliwa na                kikundi cha Rosalina Johanes kutoka Nyarusurya  ambao                walizawadiwa Shilingi 300,000/= na nafasi ya tano hadi ya                kumi walizawadiwa kifuta jasho cha Shilingi 200,000/= kila                kikundi ambavyo ni kikundi cha Khadija Simon kutoka                Nyarusurya, Debora Malima kutoka Bweri, Winfrida Majinge                kutoka Bukabwa, Tatu Siagi kutoka Kinesi, Justina                Kambarage kutoka Kinesi,  na Siwema Doto kutoka Majengo.
        
Jumla ya vikundi 90                vilijitokeza kushiliki mbio hizo za makasia chini ya                udhamini wa bia ya Balimi Extra Lager.
        Akizungumza wakati wa                kukabidhi zawadi Meneja matukio wa wa TBL Kanda ya Ziwa,                Erick Mwayela aliwashukuru wakazi wa Mara kwa kujitokeza                kwa wingi katika mashindano hayo ambapo pia aliwapongeza                walishinda na kupata nafasi ya kuwakilisha Mkoa kwenye                fainali za Kanda Desemba 6, Mwaka huu na kuwaomba ambao                hawakufanikiwa wakajipange kwa mwaka ujao.
        Fainali za Kanda za mbio                za mitumbwi zijulikanazo kama "Balimi Boat Race 2014"                zinatarajiwa kufanyika  Desemba 6, mwaka huu jijini Mwanza                katika ufukwe wa Mwaloni.
        
Comments
Post a Comment