Mkali wa Bongo fleva,              Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond akipozi.
        ANAITWA Nasibu Abdul au              maarufu kwa jina la Diamond. Alizaliwa saa kumi na moja              jioni ya Oktoba 2, 1989 katika Hospitali ya Amana iliyopo              Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Wazazi wake walimpa              jina la Nasibu wakiamini ni la bahati.
        Diamond aliongea hivi              karibuni na safu hii ya Mjue Huyu ambapo aliweka wazi mambo              mengi ya maisha yake. Diamond akiwa hajapata ufahamu, yaani              bado mdogo, wazazi wake walitengana kwa sababu ambazo bado              hazijawa wazi na baba yake kumuacha na mama.
        Kufuatia hali hiyo,              ilibidi mama yake ahamie kwa mama yake mzazi (bibi wa              Diamond), Tandale Magharibi, Dar. Hapo ndipo yakawa makazi              ya mama huyo na mwanaye.
          
        Mnamo mwaka 1995, Diamond              alianza elimu ya awali katika Shule ya Chakula Bora iliyopo              Tandale- Uzuri. Mwaka 1996 alianza elimu ya msingi katika              Shule ya Msingi Tandale- Magharibi iliyopo jijini Dar es              Salaam.
        Mwaka 2000, Diamond akiwa              darasa la tano alianza kupenda muziki, hivyo akawa anakopi              baadhi ya nyimbo za wasanii waliokuwa wakihiti ndani na nje              ya Bongo na kuimba yeye katika maeneo mbalimbali ya Jiji la              Dar es Salaam. Kwa kuliona hilo, mama yake alianza              kumnunulia kanda za albamu za wasanii tofauti hata              kumwandikia baadhi ya nyimbo za wasanii hao ili mwanae aweze              kuzishika na kuimba kirahisi.
        Diamond alizidi kuupenda              muziki ikabidi mama yake awe anampeleka kwenye matamasha              mbalimbali ili mwanae apate nafasi ya kuimba.
        Baadhi ya ndugu walimjia juu mama                huyo wakidai anamharibu mtoto badala ya kumuhimiza masomo                anamwingiza kwenye muziki ambao walidhani haukuwa na faida                yoyote.
        
Comments
Post a Comment