GAZZA AFUNGUKA NAMNA WENGER NA ARSENAL WALIVYOMLIPIA £50,000 ZA MATIBABU


GAZZA AFUNGUKA NAMNA WENGER NA ARSENAL WALIVYOMLIPIA £50,000 ZA MATIBABU

Paul Gascoigne Gazza amefunguka kwamba klabu ya Arsenal kwa ujumla ililipa kiasi cha £50,000 ambayo ni zaidi ya millioni 100 ya Kitanzania kwa ajili ya matibabu – na sehemu kubwa ya fedha hiyo ilitolewa na kocha Arsene Wenger.
Gazza, 47, alionekana mitaani kwa mara ya kwanza hivi karibuni baada ya kupelekwa kwenye kituo cha magonjwa ya akili baada ya kushamiri kwa tabia yake ya ulevi wa kupindukia mwezi uliopita.
Kiungo huyo zamani wa England ameadithia, namna Arsenal klabu ambayo hakuwahi kuichezea Screen Shot 2014-11-24 at 3.10.56 PMwalivymsaidia katika kulipia matibabu yake.

'Nilimpigia daktari wa Arsenal Gary Lewin na nikamwambia kwamba sikuwa najisikia vyema. Akaniambia niende hosptali kwa sababu alihofia ni  pneumonia. Wenger akakubali kulipa kiasi cha £28,000 kulipia matibabu yangu. Arsenal kama klabu ikatoa kiasi cha £22,000 nilipokuwa nafanyiwa upasuaji wa hips.'

Lakini, wakati Spurs ilipokuwa ikicheza na Real Madrid katika Champions League aliambiwa na klabu yake ya zamani kwamba itabidi alipe ili kuingia uwanja wa White Hart Lane.
'Nilitaka kuangalia mchezo wa Spurs vs Madrid na nikaishia kuambiwa kwamba walikuwa na tiketi 2 tu za £60. Nilipaswa kwenda kukaa kwenye sehemu ya watu maalum lakini nikaishiwa kuambiwa nilipe."

Gazza kwa sasa aemrudi kwenye afya yake na ameahidi kujirekebisha.



Comments