Mabondia Sweet Kalulu wa                Dar es Salaam kushoto na Zumba Kukwe kulia na katikati ni                mwandaaji wa pambano hilo George Nyasalu akishuhudia                mabondia hao baada ya kupima uzito na afya jana. 
        Na John Gagarini, Kibaha
        BONDIA Zumba Kukwe wa                Maili Moja wilayani Kibaha Mkoani Pwani ambaye leo                anapambana na bondia Sweet Kalulu amesema kuwa lengo lake                kubwa ni kupambana na Thomas Mashali au Kalama Nyilawila.
        Akizungumza na waandishi                wa habari jana mjini Kibaha wakati wakipima uzito na                kupima afya kwenye ukumbi wa Container Bar alisema kuwa                leo atamshinda mpinzani wake raundi ya tatu.
        Kukwe alisema kuwa                kwenye pambano lake la leo anatarajia kufanya vizuri kwa                kumpiga mpinzani wake na kuwapa raha wapenzi wa ngumi wa                mkoa wa Pwani.
        "Nimejipanga vizuri                kwenye pambano langu na sitawaangusha wapenzi wangu kwani                niko kwenye uwanja wa nyumbani, naangalia mbele zaidi                ninaowataka ni Mashali au Nyilawila," alisema Kukwe.
        Aidha alisema kuwa                anatarajia kuiweka Pwani kwenye ramani ya mchezo huo wa                ngumi hivyo malengo yake ni kupambana na mabingwa wa                Tanzania.
        "Najiamini kuwa nina                uwezo na baada ya pambano la leo safari yangu ya kuanza                kutamba kwenye ulimwengu wa ngumi itaanza na nitahakikisha                ngumi inakuwa juu mkoani Pwani," alisema Kukwe.
        Kwa upande wake Kalulu                alisema kuwa yeye hana maneno mengi anachosubiri ni muda                tu ufike na kila mtu atajua  nini kilichomleta Kibaha                kwnai anauwezo.
        Naye muandaaji wa                pambano hilo George Nyasulu alisema kuwa lengo la kuandaa                pambano hilo ni kuwahamasisha vijana wanaopenda mchezo huo                kujitokeza ili kucheza mchezo huo.
        Nyasulu alisema kuwa huo                ni mwanzo kwani baadaye ataandaa mapambano mengi zaidi na                nia ni kutoa bingwa wa ngumi Taifa kwani vijana wana                uwezo.Jumla ya mapambano saba ya utangulizi yatachezwa.
        .jpg)
Comments
Post a Comment