TOTTENHAM imeifunga Brighton 2-0 na kutinga hatua ya robo fainali ya Capital One huku Southampton nayo ikiifunga Stoke City 3-2.
Magoli ya Tottenham yalifungwa na Erik Lamela dakika ya 54 Harry Kane dakika ya 74.
Kwa upande wa Southampton Graziano Pelle alifunga dakika ya 6 na Shane Long akatupia la pili dakika ya 31 lakini Stoke wakazawazisha kwa mabao ya Steven Nzonzi dakika ya 49 na Mame Biram Diouf kunako dakika ya 82.
Zikiwa zimesalia dakika mbili mpira kumalizika Graziano Pelle akaifungia Southampton bao la ushini.
Comments
Post a Comment