Mwaka 1990 alizaliwa mtoto wa ajabu huko Marekani. Matthew          Stepanek,mtoto aliyewashangaza wamarekani wengi.Stepanek aliishi          miaka 13 tu Duniani.Kabla umauti kumkuta akiwa na umri huo wa          miaka 13 alishatunga Vitabu bora vitano vya mashairi.Wamarekani          walikua wakimuita 'peace advocate'(wakili wa amani) kutokana na          mashairi yake yaliolenga hasa kwenye Amani,Umoja na Mshikamano.          Mashairi yake yaliwasisimua watu wengi wakiwamo watu maarufu          kama Oprah Winfrey, Larry King.Lakini zaidi alikua Jimmy          Carter,Rais wa 39 wa marekani.Carter alidiriki kusema "katika          maisha yangu yote sijawai kumshuhudia mtu wa ajabu kama          Stepanek".Jimmy Carter alikua muumini mkubwa wa mashairi ya          Stepanek yaliyohamasisha umoja baina ya watu wa Marekani. "Unity          is strength.when there is teamwork and collaboration,wonderful          things can be achieved".(Umoja ni nguvu.Kila kwenye ushirikiano          na kufanya kazi kwa umoja,Mambo mazuri yanaweza kufikiwa).Hii ni          moja ya kauli zake pendwa na ya kukumbukwa ya Stepanek iliyohusu          umoja.
          Huo ni Ubongo wa mtoto aliyeishi kwa miaka 13 tu lakini          unashinda bongo za watu wengi wenye umri mkubwa.Nashukuru Mungu          nilikua mmoja wa watu walioshuhudia mechi ya Simba na Prisons          katika uwanja wa Sokoine.Wakati nasafiri kuelekea mbeya mpaka          naangalia dakika 90 za mechi hiyo niligundua kuwa Simba ina          tatizo moja tu la kukosa umoja.Simba imekosa hekima aliyekuwa          nayo mtoto mdogo Stepenak.Simba haina umoja kuanzia kwa          viongozi,Wanachama,Benchi la ufundi mpaka wachezaji.
          Benchi la ufundi la simba bila shaka limekosa mawasiliano          mazuri.Wakati mechi ikiendelea kuna muda niliona Phiri na          msaidizi wake Matola wanapishana kauli.Napata mashaka kama          maamuzi ya kiufundi kama yanatolewa na benchi nzima au mtu mmoja          pekee.Tangu nianze kushuhudia soka sijawai ona mabadiliko mabovu          mwalimu anafanya kama aliyoyafanya phiri.Kwa kumuingiza kiemba          na kutoka kwa Ndemla pale phiri alizidiwa akili na mamilioni ya          watanzania. Kuna muda naona kabisa Phiri anafanya maaumizi bila          kushirikisha benchi lake la ufundi.Sidhani kama Matola aliridhia          mabadiliko yale mabovu yaliyofanywa na kocha phiri.Phiri anaweza          kuwa kocha mzuri kuliko Matola,Lakini Matola anawajua wachezaji          wa simba vizuri kuliko Phiri.Wachezaji wengi wa simba wamefika          hapo walipo kwa nguvu za Matola.Phiri anachopaswa kufahamu kuwa          Matola ana nguvu kubwa ndani ya kikosi cha Simba.Lakini pia kuna          tetesi ndani ya timu hiyo ya kuwa kocha huyo msaidizi anahusika          kuigawa timu hiyo kupitia baadhi ya wachezaji,nilipomuuliza          kocha huyo alikataa katakata,lakini lisemwalo lipo kama halipo          basi li njiani.Kitu cha msingi ni kumaliza tofauti zilizopo          ndani ya benchi la ufundi.Lazima kuwepo na umoja, ushirikiano na          mawasiliano mazuri kati ya kocha na wasaidizi wake.
          
 Nikihama kwenye benchi la ufundi nagundua pia wachezaji wa          simba pia wamegawanyika.Kuna siku niliandika kuhusu simba          walivyokosa muunganiko 'chemistry'.Lakini wakati wa mechi yao na          Prisons nikagundua kuna mgawanyiko zaidi ya 'chemistry' ndani ya          timu hiyo.Nilianza kugundua tu wakati Singano anatoka kupisha          Haruna chanongo.Jicho la chanongo liliniambia kuna kitu          kinaendelea ndani ya kichwa cha Singano.Pia machozi ya Okwi na          Jonas Mkude kuna kitu yalikua yanamaanisha.Waswahili wanasema          'ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo'.Jicho la chanongo          kwa Singano,Machozi ya okwi na mkude,Pia kujituma kwa wachezaji          wachache uwanjani kunanifanya niamini kabisa kuna kitu          kinaendelea baina ya wachezaji wa simba.Niliposikia Amri kiemba          amesimamishwa Simba wala sikushangaa,Lakini bado nawaza kama          Singano nae ataendelea kuwa mchezaji wa Simba.Wachezaji wa simba          waliopo wanaonekana hawapo tayari kufanya kazi pamoja.Wachezaji          hao licha ya kutoelewana ndani ya uwanja wanaonekana hawaelewani          zaidi nje ya uwanja.
          Nikirudi kwa viongozi wa simba nahisi huko ndipo matatizo          yanapoanzia.Kuna viongozi Simba wanaonekana kuwa na sauti kubwa          ndani ya timu kuliko vyeo walivyo navyo.Siku hizi yupo kiongozi          ambaye anatoa taarifa zote za simba ingawa si msemaji wa          simba.Msemaji ni yeye,Mwenyekiti wa kamati ya ufundi ni yeye na          mara nyingine huvaa viatu hata vya Raisi wa klabu.Kuna muda          nafikiria nguvu ya Raisi wa simba ndani ya timu hiyo.Nahisi kuna          watu wana nguvu zaidi ya Raisi huyo wa simba.Pia kuna taarifa          nilizipata za kutokuwa na maelewano kati ya viongozi wawili wa          juu wa simba.Sasa kama baba na mama hawaelewani ndani ya nyumba          watoto ndani ya nyumba hiyo wataanzaje kuelewana?.Wachawi wakuu          wa simba ni viongozi wenyewe.Kutoelewana kwao ndio kunaleta          kuhujumiana.
          Kiukweli hali ya simba si nzuri,hali hiyo inapelekea hata          kuchukiana baina ya wanachama wa matawi ya timu hiyo.Viongozi wa          simba inabidi wawekane sawa na kila mmoja ajue mipaka ya uongozi          wake sambamba na kushirikiana na viongozi wengine na kuvunja          makundi yaliyopo ndani ya timu hiyo.Kuelewana kwa viongozi          kutaleta maelewano baina ya wanachama,benchi la ufundi na hata          wachezaji.Biblia yangu inaniambia hata Mungu hupendezwa na watu          wanaokaa pamoja na kufanya kazi kwa umoja.Kama viongozi hao          wanaona tabu kusoma biblia yangu basi wakasome mashairi ya          umuhimu wa umoja ya Stepanek yaliyomshangaza Raisi Jimmy Carter.
          Na ALLEN KAIJAGE
          Kaijagejr@gmail.com
          0655106767
Comments
Post a Comment