ISHA Mashauzi ambaye anashikilia taji la mwimbaji bora kike wa taarab kwa mujibu wa tuzo za Kili Tanzania Music Awards, Jumamosi iliyopita alidhihirisha ni kwanini alistahili tuzo hiyo.
Lakini Isha alionyesha pia ni kwanini alistahili tuzo ya mburudishaji bora wa kike ambayo nayo aliizoa miezi kadhaa iliyopita wakati tuzo za Kili zilipotolewa.
Isha alikuwa mmoja wa wasanii waliopewa ya kuburudisha kwenye tamasha la Siku ya Msanii lililofanyika Mlimani City Jumamosi iliyopita na akaitumia vema nafasi hiyo adhimu.
Akiwa msanii pekee wa taarab kuburudisha kwenye tamasha hilo, Isha akaangusha burudani safi iliyokidhi na kukonga nyoyo za watu waliofuruika ukumbini.
Pata picha 10.
Comments
Post a Comment