Na Bertha Lumala, Dar es Salaam
          KLABU ya Ndanda FC licha ya kufanya vibaya katika mechi za          mwanzo wa msimu huu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL),          imeweka rekodi katika ligi hiyo.
          Rekodi ya kwanza ya timu hiyo yenye maskani yake Masasi, Mtwara,          ni timu pekee iliyofunga goli katika mechji zote nne za kwanza          msimu huu. Hakuna timu nyingine iliyofanikiwa kufunga goli          katika mechi zote nne.
          Pili, ni timu pekee iliyofungwa goli walau moja katika mechi          zote nne za awali. Ndanda FC ilianza kwa kuishindilia Stand          United mabao 4-1 kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga          kabla ya kufungwa 3-1 na Mtibwa Sugar, 2-1 na Coastal Union na          3-1 na Ruvu Shooting.
          Nne, ni timu pekee iliyopoteza mechi nne mfululizo. Baada ya          kufungwa 1-0 nyumbani na Mgambo Shooting katika mechi ya raundi          ya tano.
          Simba SC imeweka rekodi kwa kuwa timu pekee iliyotoka sare tano          mfululizo katika mechi zote tano za awali msimu huu baada ya          kutoka 2-2 na Coastal Union, 1-1 na Stand United, 1-1 na Polisi          Morogoro, 0-0 na Yanga kabla ya sare ya 1-1 na Prisons          iliyowafanya makocha wa timu hiyo wapewe sharti la kushinda          mechi mbili zijazo dhidi ya Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting,          vinginevyo watatimuliwa.
Comments
Post a Comment