Wenger amebakisha miaka miwili na nusu katika mkataba wake wa sasa, lakini anaweza kufunga virago mwisho wa msimu kama the Gunners itamaliza Premier League bila taji na kukosa moja kati ya nafasi nne za juu.
Clement, 42, amekuwa msaidizi wa Carlo Ancelotti wakati Mtaliano huyo akipata mafanikio Stamford Bridge, Paris Saint Germain na sasa Madrid, na anaelezwa kuwa mmoja kati ya makocha bora katika dunia ya soka.
Mwingereza huyo hajashika nafasi ya juu katika klabu yoyote, lakini asili yake ya kufanya kazi na baadhi ya nyota wa daraja la juu duniani wakati akiwa Ufaransa na Hispania inamuweka katika nafasi ya kupewa mikoba the Gunners.
Comments
Post a Comment