MANYIKA ALIA KAMA KAFIWA….



MANYIKA ALIA KAMA KAFIWA….

Na Mwandishi Wetu Mbeya

manyika

KIPA kinda wa Simba, Peter Manyika Jr amejikuta akilia kama mfiwa baada ya kufungwa goli la usiku katika sare ya bao moja dhidi ya Tanzania Prisons mjini hapa jana.
Goli la winga mtokea benchini Hamis Maingo dakika moja kabla ya mechi kumalizika liliipa sare ya usiku Prisons kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini hapa jana na kumuacha kipa huyo akiangua kilio baada ya kuikosesha timu yake ushindi wa kwanza msimu huu.
Baada ya mechi kumalizika kipa nambari moja Simba Ivo Mapunda alimfuata Manyika Jr kumkumbatia huku akimwambia "vumilia mdogo wangu, ndivyo mpira ulivyo."
Goli la Simba lilifungwa na mshambuliaji kutoka Uganda, Emmnuel Okwi dakika nne tu baada ya kipyenga cha refa Othman Lazi kutoka Morogoro kupulizwa.
Goli walilofingwa lilionekana kumuuma zaidi Manyika Jr kwani wakati wenyeji wanafanya shambulizi, alikuwa amelala amelala kuashiria kuumia ikiwa ni janja ya kupoteza muda lakini baada y mfungaji kukaribia lango, kipa huyo aliyedaka mechi ya watani wiki mbili zilizopita, aliinuka lakini tayari alikuwa ameshachelewa.
Ni goli la kwanza kwa kipa huyo msimu huu huku makipa chaguo la kwanza Ivo na chaguo la pili Hussein Sharrif 'Casillas' wakifungwa magoli mawili kila mmoja.
Kwa matokeo hayo, Simba inakamata nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi tano baada ya kuambulia sare katika mechi zote tano za mwanzo wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Mechi ya jana pia ilikuwa ya 11 kwa wekundu kucheza ligi kuu bila kupata ushindi tangu waifunge Ruvu Shooting mabao 3-2 miezi saba iliyopita.



Comments