HALI ni tete kwa Manchester City – wamevuliwa taji la Capital One kwa kuchukua kichapo cha 2-0 kutoka kwa Newcastle United huku wakiwa na mtihani mzito Jumapili hii kwenye Ligi Kuu pale watakapoikaribisha Manchester United.
Kinda wa miaka 18 Rolando Aarons aliitanguliza Newcastle kwa bao la mapema kunako dakika ya 5 huku City wakijaribu kuchomoa bila mafanikio.
Ilipotimu dakika ya 75, jahazi la City likazidi kuzama baada mshambuliaji Moussa Sissoko alipokwamisha wavuni bao la pili na kuipeleka Newcastle hatua robo fainali kukabiliana na Tottenham.
MANCHESTER CITY: (4-2-3-1) Caballero 5.5; Sagna 6, Demichelis 6, Mangala 5.5, Kolarov 6; Fernandinho 5.5, Toure 6 (Navas59mins 6) ; Milner 6.5, Jovetic 5.5, Silva 6 (Nasri 8mins 7 (Aguero 69mins 6 )); Dzeko 5.5
NEWCASTLE UNITED: (4-1-4-1) Elliot 6; Janmaat 6.5 (Sissoko 64mins 7), Coloccini 7, Dummett 6.5, Haidara 7; Abeid 7; Obertan 7, Taylor 7.5, Colback 6.5, Aarons 7 (Ameobi 45mins 6.5); Armstrong 6 (Riviere 64mins 6).
Comments
Post a Comment