Manchester, England,
          Jose Mourinho alikwepa kumzungumzia mwamuzi, Phil Dowd ambaye          alichezesha mchezo wa jana kati ya timu yake ya Chelsea na          Manchester United katika uwanja wa Old Trafford. Chelsea          iliongoza kwa bao la mshambulizi, Didier Drogba katika dakika ya          53 na ilionekana kama timu hiyo ingeondoka na pointi tatu kabla          ya Robbin Van Persie kuisawazishia United katika dakika ya          mwisho ya mchezo na kutengeneza sare ya kufungana bao 1-1.
          
          " Kwa sasa tuna nafasi ndogo kutokana na makosa yetu ama          kutokana na makosa ya mwamuzi. Kama nikisema kilicho moyoni          mwamgu nitakuwa katika matatizo. Nimechagua kutozungumzia          kitendo cha Ivanovic kutolewa kwa kadi nyekundu. Kuna mambo          mengi yalikwenda kinyume, na matokeo hayakuwa mazuri kwa upande          wetu lakini yanakubalika" alisema, ' The Special One'
Chelsea imeendelea kujidhatiti katika msimamo wa ligi kuu ya          England, baada ya kucheza michezo tisa ikiwemo dhidi ya timu za          Everton, Manchester City na Arsenal, timu hiyo imekusanya pointi          23, pointi nne zaidi ya Southampton walio katika nafasi ya pili,          huku wakiwa wamewaacha United kwa pointi kumi. Chelsea          haijapoteza mchezo wowote msimu huu na jambo hilo limemfanya.,          Jose kuwasifu wachezaji wake licha ya kutoshinda Old Trafford.
          
          " Nina furaha kutokana na timu yangu kucheza vizuri, si rajhisi          kucheza dhidi ya United ambao wanacheza mchezo wa kusogeleana          huku wakitumia mbinu za kushambulia kwa kushtukiza. Tungeweza          kufunga mabao zaidi hasa ile nafasi iliyopotezwa na Hazard.          Najivunia wachezaji wangu".
Drogba alifunga bao katika mchezo wake wa 350 akiiwakilisha Chelsea huku likiwa bao la kwanza msimu huu kwa mchezaji huyo katika ligi kuu. Mchezaji huyo raia wa Ivory Coast alicheza kwa nguvu muda wote wa dakika 90 ambazo Chelsea ilikosa huduma ya washambuliaji wake, Diego Costa na Loic Remy;
" Hakuweza kufanya mazoezi na kucheza kwa dakika 90 kama alivyocheza leo ( jana) Nina furaha kumuona akifunga bao, Drogba tayari amefunga mabao mengi kama hili alilofunga"
Comments
Post a Comment