REAL Madrid wamechanua kwenye La Liga baada ya kuwachapa watani wao wa jadi Barcelona 3-1 na kuzidi kupunguza pengo baina yao ambapo sasa wanatenganishwa na pointi moja tu.
Neymar aliwanyamazisha wenyeji kwa bao la dakika 3 baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Luis Suarez ambaye alikuwa anaichezea kwa mara kwanza Barcelona tangu afungiwe kwa kosa la kumng'ata mchezaji kwenye World Cup.
Lakini Ronaldo alirejesha utulivu dakika ya 35 pale alipoisawazishia Real Madrid kwa penalti.
Beki wa kati wa Real Madrid, Pepe akafunga bao la pili dakika 50 kabla ya Karim Benzema kufunga kitabu cha magoli dakika ya 61.
Supastaa wa Barcelona Lionel Messi alishindwa kuisadia timu yake huku mpinzani wake mkubwa Cristiano Ronaldo akiendelea kuwa mtambo wa magoli.
Angalia umati wa mashabiki waliokuwa nje ya uwanja kuilaki Real Madrid ikiwasili kuikabili Barcelona
Comments
Post a Comment