"Kitu cha kwanza na muhimu kwenye vita ni pesa,Pesa          inamaanisha vitu vingine vyote,Askari,bunduki na risasi".Maneno          ya hekima ya miongoni mwa wanawake majasiri kuwai kutokea          Duniani.Ida Tarbell,Mwalimu na mwandishi wa habari za siasa wa          zamani wa marekani.Miaka sabini sasa tangu Mungu amchukue,Lakini          maneno yake yanaishi mpaka leo.Pesa ndio kila kitu bwana.Tafuta          pesa kwanza,Vingine vitatengenezwa na pesa uliyopata.Pesa ni          silaha kuu ya kumshinda adui yako.Hakuna kitu bora          kinachoendeshwa bila pesa.Kwa ufupi Pesa ndio alama kuu ya          mafanikio.Hata kwenye soka pesa inacheza zaidi kuliko miguu ya          wachezaji.
          Mpira wa leo umetawaliwa na watu wenye pesa zao, Lakshmi Mittal,          Alisher Usmanov, Roman Abramovich ni miongoni mwa mabilionea          Duniani wanaomiliki na kudhamini vilabu mbalimbali kwenye ligi          kuu ya England. Ligi ya uingereza inapendeza kutokana na mchango          wa vigogo hawa wenye pesa zao.Bila jeuri ya pesa kusingekuwa na          ubingwa wa Chelsea wala Manchester City.Makombe ya Chelsea          yamenunuliwa na Pesa chafu za Roman Abramovich,Pesa hizo hizo          ndio zimeleta mapinduzi ya soka nchini Uingereza.Ni jambo la          kawaida sasa kuona vilabu vikongwe uingereza Liverpool na          Manchester united vikitupwa mbali na mbio za ubingwa.Hakika pesa          imetengeneza ligi kuu ya uingereza.
          Patrice Motsepe, Kaizer Motuang, Moise Chapwe, Irvin Khoza ni          miongoni mwa wamiliki wa vilabu maarufu barani Afrika.Pia watu          hao ni miongoni mwa matajiri wakubwa Afrika.Ukiachana na Moize          Chapwe waliobaki watatu yaani Patrice Motsepe, Kaizer Motuang,          Irvin Khoza wote wanamiliki na kudhamini vilabu vya nchi ya          Afrika kusini.Kwanini ligi kuu ya Afrika kusini isiwe ligi bora          barani Afrika?.Pesa za kina Patrice Motsepe, Kaizer Motuang,          Irvin Khoza ndio chagizo kubwa ya ligi hiyo kua bora na yenye          mvuto kwenye bara letu pendwa la Afrika.
          
 Hakika tangu kuzaliwa kwangu sijawai kuona ligi ya Tanzania          inapendeza kama miaka hii miwili ya karibu.Mvuto wa ligi          unaongezeka kadiri miaka inavyosonga.Ligi kuu ya mwaka jana          ilikua nzuri kuliko ya mwaka juzi,pia bila shaka ya mwaka huu          mpaka ilipofika inaelekea kunoga kuliko ya mwaka jana.Nyuma ya          kuimalika kwa ligi hii kuna watu na pesa zao wamesimama.Wapo          wengi ila leo napenda kuutambua mchango wa Bakhresa na          Binslum.Kama ningekuwa tff ningeandaa tuzo kwa ajili ya watu          hawa.Bakhresa na Binslum ni mikongoni mwa matajiri wachache          wenye mapenzi ya dhati na mpira wetu.Hawa watu bila shaka wana          malengo ya dhati kukuza soka la Bongo.Kaizer chief, si timu          kongwe kama Simba na Yanga,ila ni timu bora kuliko simba na          Yanga.Kaizer Motuang alipata maono ya kuanzisha kaizer chiefs          mwaka 1970,Bakhresa alivyoanzisha Azam ni kama Kaizer          alivyoanzisha Kaizer Chiefs.Mapinduzi ya soka la Afrika Kusini          yalianzia kwa Kaizer chiefs kama Tanzania yalivyoanzia kwa          bakhresa.Licha ya bakhresa kumiliki timu ya azam pia tajiri huyo          ametoa udhamini kwa klabu zote zinazoshiriki ligi kuu Tanzania          bara.Pesa za bakhresa zimehamasisha miguu ya wachezaji wengi          wanaoshiriki ligi kuu.Pesa zake zimepunguza ukata uliokua          unazikabiri timu zisizo na wadhamini.Hakika pesa za Bakhresa          zinacheza ligi kuu yenye mvuto.Ukiachana na Bakhresa kuna mtu          anaitwa Binslum, Binslum ametumia zaidi ya million 450 kuwekeza          kwenye soka.
          naye amefanya kwa sehemu yake.Ametoa udhamini wa vilabu vitatu          Tanzania bara,Tena kati ya vilabu hivyo vitatu ,viwili ndio          kwanza vimepanda ligi kuu msimu huu.Stand united na Ndanda          zimepanda ligi kuu huku zikijihakikishia mamilioni kutoka kwa          bakhresa na Binslum.Hii ni tofauti na zamani timu inapanda          daraja inakosa hata pa kuanzia,Jambo hili lilipelekea timu kubwa          kutumia udhaifu wa timu ndogo kupenyeza kirusi kinachoitwa          rushwa.Hata kama Binslum na Bakhresa hawajamaliza tatizo la          rushwa lakini watakua wamepunguza kwa asilimia kubwa.
          
 Kama kungekua na bakhresa watatu na binslum watano hakika ligi          yetu na soka letu kwa ujumla lingekua mbali. "Hivi ndivyo          nnavyofikiri kuhusu pesa yangu,pesa yangu ni kama          askari,nawatuma vitani kila siku nataka iende ikakamate mateka          na kuwarudisha nyumbani".Maneno ya bilionea jeuri Duniani,Raia          wa Canada Kevin O'Leary. Matajiri na Makampuni makubwa inabidi          wajifunze kuwekeza na kujitangaza kupitia soka.Soka ni biashara          nzuri,Bakhresa, Patrice Motsepe, Kaizer Motuang, Moise Chapwe na          Irvin Khoza wanajua umuhimu wa kutumia askari pesa kupata          mateka(faida) kwenye vita ya soka(biashara).Bila shaka Bakhresa          na Binslum walimuelewa vizuri Kevin O'Leary.
          Licha ya Bakhresa na Binslum kusaidia soka letu bali pia na wao          kuna faida wanapata kupitia kutangaza biashara zao.Watanzania          wengi wanapenda soka,Bidhaa za Binslum na Bakhresa zinapendwa na          watu wengi kwasababu ya kujitangaza kwao haswa kupitia soka.          Wito wangu kwa matajiri na makampuni makubwa kuamka na kuanza          kuwekeza kwenye soka.Uwekezaji wao kwenye soka utakua na faida          kwa Taifa lao pia na kwao binafsi.Bakhresa na Binslum wanapiga          shuti moja na kufunga magoli mawili,yaani wanatumia pesa zao          kwenye soka kufunga magoli mawili,la kwanza wanafunga kwa soka          la Tanzania na la pili kwenye biashara zao.Tusiwaache Binslum na          Bakhresa pekee wafaidi akili za Kevin O'Leary kwenye          vita(biashara) ya soka la Bongo.Tusiwaache watu hawa watumie          peke yao ubongo wa Kevin O'Leary kufunga magoli mawili kwa shuti          moja.
          Na
          Allen kaijage
          0655106767
          kaijagejr@gmail.com
Comments
Post a Comment