Baada ya kuanza vibaya kampeni ya kurudi ligi kuu msimu ujao kwa kupoteza mechi zao nne za mwanzo katika ligi ya daraja la kwanza, timu ya African Lyon ya Dar es Salaam imemtimua kocha wao Jummane Chale na sasa ipo katika hatua za mwisho za kumrudisha tena kocha wa kireno Eduardo Filipe Arroja Almeida.
African Lyon ambao wamedhamiria kurudi ligi kuu msimu ujao, wanamrudisha Eduardo Filipe Arroja Almeida ambaye aliwahi kuifundisha timu hiyo katika msimu wa 2009/10 anatarajiwa kutua nchini ndani ya siku chache zijazo.
Eduardo Filipe Arroja Almeida anatokea katika klabu ya Atlético Clube S.C amewahi kuvifundisha vilab vifuatavyo:
Sport Alenquer and Benfica (2000/2001) 1
Sport Lisboa and Benfica (2001/2004) U 16 – Portugal
U.F.C. Almeirim (2004/2005) U 19 – Portugal
Atletico Clube Cacem (2005/2007) 3
South China (2007/2008) Hong Kong Premier League
Clube F. Estrela Amadora (2008/2009) U-17
Atletico Clube Cacem (2008/2009) 3
African Lyon F.C (2009/2010) Premier League
Real Sport Clube (2010/2011) (6 months) Second National Division
Associação Naval 1o Maio(2010/2012) Premier League
st District Division- Portugal
rd National Division – Portugal
rd National Division – Portugal
Comments
Post a Comment