Mshambuliaji kutoka nchini Uruguay Luis Suarez,                bado ana hamu ya kuwa sehemu ya kikosi cha FC Barcelona                ambacho kwa msimu huu kipo chini ya meneja kutoka nchini                Hispania Luis Enrique Martínez García.
        Suarez,                anaetumikia adhabu ya kufungiwa kucheza soka katika                michuano ya kiushindani kwa kipindi cha miezi minne,                ameonyesha hamu ya kutaka kurejea na kujiunga na wachezaji                wengine wa FC Barcelona ambapo itakuwa ni mara yake ya                kwanza baada ya kusajiliwa akitokea Liverpool, kufutia                juhudi anazo zionyesha katika mazoezi pamoja na michezo ya                kujipima nguvu ambayo inakihusisha kikosi cha Barcelona                B. 
                      Usiku wa                  kuamkia hii leo, mshambuliaji huyo alieacha gumzo nchini                  Brazil baada ya kumng'ata beki wa kati wa timu ya taifa                  ya Italia na klabu ya Juventus Giorgio Chiellini,                  alicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya                  Indonesia chini ya umri wa miaka 19 ambapo Barcelona B                  imeichapa Indonesia kwa mabao 6 kwa sifuri. 
                          Kocha                    wa Barcelona Luis Enrique amesema alitaka Suarez                    kucheza mchezo huo ili kuwa katika hali ya hamasa ya                    kimchezo, kabla ya kurejea uwanjani rasmi mwishoni mwa                    mwezi oktoba. 
                              Suarez anaruhusiwa kushiriki michezo ya                      kirafiki pekee, na hatashiriki michuano ya ligi ya                      nchini Hispania La Lila mpaka tarehe 24 mwezi oktoba                      ambapo Barcelona itakutana na Real Madrid
              
Comments
Post a Comment