FILAMU mpya ya                  muimbaji wa nyimbo za Injili, Jennifer Mgendi iitwayo                  'Mama Mkwe' inatarajiwa kuigizwa sokoni siku ya Alhamisi                  baada ya kukwama kuachiwa jana Jumatatu kama ilivyokuwa                  imepangwa.
                        Aidha Muinjilisti huyo                  amewataka mashabiki wake wasiikose kupata darasa la                  kutosha.
                Jennifer alisema filamu                  hiyo itaachiwa rasmi Septemba 25 baada ya jana kukwama                  kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake ikiwa ni wiki kadhaa                  tangu kumalizika kurekodiwa kwake na kusema kwa ujumbe                  uliopo ndani yake, mashabiki hawapaswi kuikosa. 
                Muimbaji huyo alisema,                  kisa cha Mama anayeingilia ndoa ya mwanae wa kiume                  akitaka kupatiwa mjukuu ni mambo ambayo yamekuwa                  yakiwakumba wanajamii wengi na kusambaratisha ndoa zao                  bila kutaka.
                              "Ni mambo yanayotokea                  ndaniya jamii na kuwaachia watu machungu, sasa waigizaji                  wameonyesha uhalisia wa mambo namna ndoa nyingi                  zinavyosambaratika kwa sababu ya mambo kama hayo,"                  alisema.
                Katika filamu hiyo,                  Jennifer ameigiza na wasanii wengine wakali kama kina                  Mussa Banzi, Bahati Bukuku, Christine Matai, Bibi Esther                  na wengine.
                              "Itakuwa mtaani Alhamisi,                  mashabiki wasikose kuona uhondo huu. Mama Mkwe ni zaidi                  ya kazi zangu za nyuma kwa namna ilivyosukwa na                  kutendewa haki na wasanii walioigiza," alitamba                  Jennifer.
               
Comments
Post a Comment