MANCHESTER UNITED YAJA MDOGO MDOGO …yachukua pointi 3 kwa West Ham, Rooney hakui



MANCHESTER UNITED YAJA MDOGO MDOGO …yachukua pointi 3 kwa West Ham, Rooney hakui
MANCHESTER UNITED YAJA MDOGO MDOGO …yachukua pointi 3 kwa            West Ham, Rooney hakui

WAYNE Rooney amefunga lakini akaambulia kadi nyekundu wakati Manchseter United ikipata ushindi wake wa pili kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuilaza West Ham 2-1 kwenye dimba la Old Trafford.

Baada ya kipigo cha kuduwaza cha 5-3 kutoka kwa Leicester City katika mchezo uliopita, United ikaanza kwa kishindo baada ya Rooney kuandika bao la kwanza dakika ya 2 kufuatia krosi safi kutoka kwa Rafael.

Robin van Persie akaindikia United bao la 2 dakika ya 22 kabla Diafra Sakho kuipatia West Ham bao pekee dakika ya 37.

Manchester United striker Wayne Rooney, centre, is                  shown a red card by referee Lee Mason

Katika kipindi cha pili nahodha wa United Wayne Rooney akalambwa kadi nyekundu baada ya kumpiga teke Stewart Downing – rafu ya kijinga inayomfanya mchezaji huyo wa England afungiwe kwa mechi tatu.

Manchester United's Wayne Rooney takes down Stewart                  Downing of West Ham and receives a red card

Manchester United (4-1-2-1-2): De Gea 6; Rafael 6, McNair 7, Rojo 6, Shaw 6; Blind 7; Herrera 7 (Valencia 74 6), Di Maria 6 (Thorpe 90 6); Rooney 4; Van Persie 7, Falcao 6 (Fletcher 65 6).

West Ham (4-3-1-2): Adrian 5; Demel 6 (Jenkinson 65 6), Tomkins 6, Reid 5, Cresswell 6; Song 5, Poyet 6, Amalfitano 6 (Cole 61 6); Downing 6: Sakho 7, E Valencia 6.



Comments