JUAN Mata amewaomba radhi mashabiki wa Manchester United kwa kiwango kibovu kwenye mchezo wao dhidi ya Leicester City na kusema anashiriki nao katika maumivu waliyoyapata baada kushindwa kuulinda uongozi wao wa mabao mawili.
United iliongoza 2-0 na baadae 3-2 kwenye uwanja wa King Power lakini ikajikuta ikichukua kichapo cha 5-3 katika mchezo ambao nyota huyo wa Hispania anauelezea kuwa ulikuwa wa kukatisha tamaa.
Mata amewaahidi mashabiki wao kuwa United itarejea na nguvu mpya katika mechi zao mbili zijazo za uwanja wa nyumbani dhidi ya West Ham na Everton.
Akiandika kwenye blog yake, Mata ambaye aliingia badala ya Angel di Maria dakika 14 kabla mpira haujaisha, alisema baada ya kusubiri mechi kwa wiki nzima, kamwe hakutegemea kukumbana Jumapili ya aina hiyo.
Comments
Post a Comment