| .jpg) | 
| Wachezaji wa Boda Boda FC na washabiki wao wakishangilia ushindi baada ya kujinyakulia kombe la virutubishi katika pambano ililofanyika katika uwanja wa Bondeni wilayani Karatu | 
Timu zenye upinzani wa jadi wilayani Karatu                mkoani Arusha za  Boda Boda FC na Young Generation  jana                zilikuwa na mpambano mkali wa mchezo  wa soka ambapo timu                ya Boda Boda iliibuka na  ushindi wa mabao 2-1.
        Mechi hiyo ambayo ilichezwa katika uwanja                wa Bondeni chini ya udhamini wa  Wizara ya Afya na Ustawi                wa jamii kitengo cha kutoa elimu ya virutubishi kwa jamii                ilishuhudiwa na wakazi wa wilaya ya Karatu wapatao 8,000                na mgeni wa heshima alikuwa Mkuu wa Polisi wa wilaya ya                Karatu (OCD) Jubileth Nyange.
        Timu zote 2 zilicheza kwa kujituma na                kushangiliwa na wapenzi wa soka ambao ni washabiki wa timu                hizo ambapo katika kipindi cha pili Boda FC ilifanikiwa                kupachika mabao 2 mfululizo na wapinzani wao wakafanikiwa                kurejesha bao moja.
        Kwa matokeo hayo timu iliyoshinda iliweza                kujipatia kombe na seti ya jezi za kisasa wakati wapinzani                wao walijipatia mipira miwili kutoka kwa mdhamini.Mratibu                wa  mchezo Allan Rwechungura kutoka taasisi ya Foot Print                alisema lengo la  mchezo huo  lilikuwa ni kutoa burudani                kwa wananchi wakati huo huo kuwapatia elimu ya lishe na                matumizi ya vyakula vilivyowekewa virutubishi,kampeni                ambayo inaendelea katika wilaya mbalimbali nchini chini ya                usimamizi wa Wizara ya Afyana Ustawi wa Jamii.
        Alisema kwa kuwa michezoni jukwaa la                kukusanya watu wengi wataandaa mashindano ya michezo                mbalimbali kwenye wilaya za hapa nchini ambapo timu                zitakazofanya vizuri zitajipatia vifaa vya michezo wakati                huo huo wananchi wataofika viwanjani kupatiwa elimu ya                lishe bora na matumizi ya virutubishi lengo likiwa  ni                kufikisha ujumbe wa wananchi wa kawaida.
        
Comments
Post a Comment