ROY KEANE AKUTANA NA TOM CLEVERLEY KUJARIBU KUMTOA MAN UNITED NA KUMHAMISHIA ASTON VILLA




ROY KEANE AKUTANA NA TOM CLEVERLEY KUJARIBU KUMTOA MAN UNITED NA KUMHAMISHIA ASTON VILLA

This is the end: The midfielder's days appear to                    be numbered at Old Trafford after management changes

TOM CLEVERLEY amekutana na kocha msaidizi wa Aston Villa kujadili suala la uhamisho wa kutimka Old Trafford.

Keane ambaye ni mmoja wa nyota waliojizolea mafanikio makubwa katika Manchester United, anajaribu kufanya kila awezalo kumtwaa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25 kwa kumpa ahadi ya kuwa chaguo la kwanza.

Cleverley ambaye tayari ana ofa ya  pauni milioni 7 kutoka kwa Aston Villa, anawaniwa pia na Everton, Hull and Valencia.

Kiungo huyo ambaye bado hajaamua ni wapi pa kwenda, angependelea zaidi kuondoka kwa mkopo kwa msimu mmoja kabla ya kutimka bure kwenye kikosi cha Louis van Gaal kiangazi kijacho.



Comments