
Marcos Rojo amapata kibali cha                kufanya kazi nchini England na ilitegemewa jumamosi hii                aanze kuitumikia United lakini taarifa kutoka UK zinasema                kwamba mchezaji huyo wa kiargentina anaweza bado asipate                ruhusa ya kuichezea klabu mpya kutokana na ugomvi wa                kisheria uliopo kati ya Sporting Lisbon na kampuni ya                Doyen Sports iliyokuwa inamiliki haki zake za usajili kwa                asilimia 75. 
                          United                        imemsajili Rojo kutoka Lisbon kwa ada ya jumla ya                        £16m lakini wamelipa £8m kwa sasa na baada                        watalipa £4m X2. Premier League hairuhusu suala la                        'umiliki wa pande 3' (Third Part Ownership) -                        mtindo ambao unaruhusiwa kwenye nchi kama Ureno                        alipotoka Rojo. Tatizo la Third Part Ownership                        liliwahi kuiletea matatizo West Ham huko nyuma                        waliposajili Carlos Tevez na Javier Alejandro                        Mascherano
                
Comments
Post a Comment