
Beki Marcos Rojo                    amelazimika kupanda ndege na kurejea jijini Madrid,                    Hispania akilazimika kusubiri kupatikana kwa visa na                    kibali cha kazi ili arejee kujiunga na timu yake mpya                    ya Manchester United.Imeelezwa                    akiwa Madrid, Rojo raia wa Argentina atafanyiwa                    mahojiano yatakayomuwezesha kupata visa hiyo.Ingawa kumekuwa na ugumu unaotokana                na suala la kesi yake inayomkabili iliyotokea miaka mitano                iliyopita baada ya kuzozana na majirani zake.
            Kwa sheria kali za                    England, inatakiwa kuwa na uhakika kuwa Rojo                    hatawasumbua majirani zake atakaoishi nao jijini                    Manchester na ikigundulika alikuwa mkorofi, basi                    anaweza kunyimwa viza na United ikamkosa.
            Hata hivyo, wakati                    Rojo akiwa Madrid, uongozi wa Man United umesisitiza                    suala hilo linakwenda ukingoni na beki huyo                    iliyemsainisha kwa pauni milioni 16 kutoka
            Sporting Lisbon ya                    Ureno, ataungana na wenzake na kuanza kazi.
          
Comments
Post a Comment