 
          
Mchezaji                      nyota wa kimataifa wa Holland na Ajax, Daley Blind.
          MANCHESTER UNITED imekubali                kulipa dau la pauni milioni 14.2 iliyohitajiwa na Ajax ili                kumsajili nyota wa kimataifa wa Holland Daley Blind.Kilichobakia sasa kwa                Blind mwenye umri wa miaka 24 ni kukubaliana na United                kuhusu maslahi yake binafsi na kwenda kufanya vipimo vya                afya.United inaamini mchezaji              huyo mwenye uwezo wa kucheza kama beki wa kushoto, beki wa              kati na kiungo mkabaji, atakamilisha usajili wake kabla              dirisha la usajil halijafungwa.
                                                                          Habari kutoka Holland zinasema ada                      iliyofikiwa ni pauni 14.2 ambapo United                      ikathibitisha kupitia akaunti yake ya Twitter kuwa                      wamekubaliana na ada hiyo na watatangaza                      kitakachojiri hapo baadae.
                                            
Comments
Post a Comment