DI MARIA ASAINI MIAKA MITANO OLD TRAFFORD NA KUSEMA HAKUNA KLABU NYINGINE YOYOTE AMBAYO INGEMFANYA AACHANE NA REAL MADRID ZAIDI YA MANCHESTER UNITED



DI MARIA ASAINI MIAKA MITANO OLD TRAFFORD NA KUSEMA HAKUNA KLABU NYINGINE YOYOTE AMBAYO INGEMFANYA AACHANE NA REAL MADRID ZAIDI YA MANCHESTER UNITED

Recruit: Manchester United announced the signing                    of Di Maria on Tuesday night

ANGEL DI MARIA hatimaye amekuwa mchezaji wa Manchester United kwa rekodi ya manunuzi Uingereza - pauni milioni 59.7 na kusema asingeweza kuiacha Real Madrid kwa klabu nyingine yoyote ile isipokuwa Manchester United.

Winga huyo wa Argentina amesaini mkataba wa miaka mitano Old Trafford na ataingiza pauni milioni 6.5 kwa mwaka baada ya kukatwa kodi. Kipato kitakachomfanya nyota huyo wa miaka 26 awe mchezaji wa pili wa United anayelipwa pesa nyingi zaidi nyuma ya Wayne Rooney.

Got him! Angel di Maria poses with Manchester                  United boss Louis van Gaal upon signing

Kauli ya Di Maria kwamba angeeicha Real Madrid kwa ajili ya United pekee, itawakera Manchster City. Mabingwa hao wa watetezi wa Barclays Premier League walimpa ofa kama hiyo Di Maria wiki iliyopita.

New motor: Di Maria poses in front of a Chevrolet                  car outside Aon Training Complex

"Hakika nina furaha kujiunga na Manchester United," alisema Di Maria.

"Nimekuwa nikifurahia muda wangu Hispania na vilabu vingi vilivutiwa nami, lakini United ni klabu pekee ya kunifanya niachane na Real Madrid," alisema Di Maria.

Long-term man: Di Maria signs on a five-year deal                  from European champions Real Madrid

Chief coup: Executive vice-chairman Ed Woodward poses                with Di Maria



Comments