UHAMISHO WA REMY KWENDA LIVERPOOL 'WASUASUA

 
 
 
 
 
Uhamisho wa pauni milioni 8.5 wa Loic Remy, 27, kutoka QPR kwenda Liverpool umeshindwa kukamilika.
Liverpool hawataki kusema kwanini uhamisho huo umeshindikana, lakini inasemekana huenda mchezaji huyo ameshindwa kupita vipimo vya afya.
Remy alisafiri hadi Marekani siku ya Jumatatu ambapo Liverpool wanafanya ziara.
Liverpool walipanga kumpa jezi namba 7 kama mkataba ungekamilika.
Remy sasa huenda akalazimika kurejea QPR.

Comments