Kocha mkuu wa Ruvu   Shooting, Mkenya Tom Alex Olaba amewaamini vijana wake chini ya umri miaka   20
  KOCHA mkuu wa Ruvu   Shooting, Mkenya Tom Alex Olaba amedhamiria kukijenga upya kikosi chake kwa   kuwapa uzoefu vijana wenye umri chini ya miaka ishirini (U-20) waliowapandisha   kutoka timu B na wale waliosajiliwa wakati wa majaribio.Ruvu Shooting   aliwafanyia majaribio wachezaji vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania   mwezi mei mwaka huu na wale waliofuzu walijiunga na timu B.Ikiwa   ni sehemu ya kuwaimarisha na kuwapa uzoefu wa kucheza ligi kuu, Olaba anawapa   nafasi ya kucheza mechi mbalimbali za kirafiki.
  Kocha huyo aliyefungwa   bao 1-0 na Azam jana katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi, jijini Dar es   salaam alisema vijana wake hawajapata uzoefu, lakini wanaonekana kucheza vizuri   na kadiri siku zinavyokwenda hofu inawatoka.
  "Ukiangalia jinsi   tulivyocheza mechi ya kirafiki na Azam fc, utagundua haraka haraka kuwa vijana   wa U-20 walikuwa na wasiwasi,". Alisema Olaba.
  
Msimi uliopita, Ruvu   Shooting walifungwa mabao 7-0 dhidi ya Yanga sc uwanja wa   Taifa
  "Kipindi cha kwanza   tulicheza vizuri sana, lakini kipindi cha pili wao wakapata goli moja. Kufungwa   kwangu,  mimi sina neno. Nina maana yangu ya kucheza ya mechi za   kirafiki".
  "Niliwaweka U-20, ndio   mara yao ya kwanza kucheza na Azam, ukiwatazama unaona walitetemeka. Azam wengi   wao ni wachezaji wa kigeni, wachezaji wangu wa U-20 wamepata uzoefu mkubwa.   Aliongeza Olaba.
  Aidha, Olaba alisema   kuwa anatarajia kucheza mechi nyingi zaidi za kujipima uwezo baada ya mwezi   mtukufu wa Ramadhani, lengo likiwa ni kukisuka kikosi kwa ajili ya ligi kuu   inayotarajia kuanza kushika kasi septemba 20 mwaka huu..
  "Nitacheza mechi nyingi   sana, hata hivi leo  ninacheza na JKT Ruvu Stars hapa kwetu Mabatini. Baada   ya sikuu ya ramadhani nitacheza mechi nyingi sana, siwezi kutaja idadi".   Aliongeza Olaba.
  "Kila kocha anapocheza   mechi za kirafiki anaona makosa, akirudi nyumbani anaenda   kurekebisha".
  Msimu uliopita, Olaba   aliyerithi mikoba ya aliyekuwa kocha mkuu na akatimkia Yanga sc, Charles   Boniface Mkwasa `Master`  aliiongoza Ruvu Shooting kushika nafasi ya 6   katika msimamo wa ligi kuu kwa kujikusanyia pointi 38   kibindoni.
Walishinda mechi 10,   walitoka sare mechi 8 na kufungwa mechi 8. Idadi ya mabao waliyofunga yalikuwa   28 na walifungwa mabao   32.
Comments
Post a Comment