Kikosi cha Mtibwa Sugar msimu                uliopita. Mlinda mlango Hussein Sharrif `Casillas`                amejiunga na Simba majira haya ya kiangazi na kusaini                mkataba wa miaka miwiliTIMU nyingi zinazoshiriki ligi                kuu soka Tanzania bara zipo katika maandalizi ya kujiwinda                na msimu mpya utakaoanza kushika kasi septemba 20 mwaka                huu.Wakata miwa wa mashamba wa Manungu,            Turiani mkoani Morogoro, Mtibwa Sugar wapo jijini Dar es            salaam kujifua katika fukwe za Koko ili kujiimarisha zaidi.
                Mtibwa Sugar chini ya kocha                mkuu, Mtanzania Mecky Mexime, msimu uliopita ilimaliza                katika nafasi ya 7 kwa kujikusanyia pointi 31 kibindoni.
        Mabingwa hao mara mbili                mfululizo wa Tanzania kwa mwaka 1999 na 2000 walishinda                mechi 7, sare 10 na kufungwa mechi 9. Walitikisa nyavu za                wapinzani mara 30 na zao kuguswa mara 31.
        Tangu itwae ubingwa miaka miwili                mfululizo (1999, 2000), Mtibwa haijawahi kuwa katika ubora                wake na kujikuta ikishika nafasi za kawaida katika                msimamo.
        Msimu uliopita walishindwa                kutamba kabisa na kuziacha timu za Azam fc, Yanga, Mbeya                City fc, Simba, Kagera Sugar na Ruvu Shooting kukaa juu                yao katika msimamo wa ligi kuu.
        Mtibwa ni timu inayoendeshwa                kikampuni na haina matatizo kama klabu za wanachama,                lakini haijawa na makali kama Azam fc na hata pacha wao                 Kagera Sugar.
        Kuelekea msimu ujao, wakata miwa                hao wa Manungu wamesema wanajifua vilivyo ili kurejesha                heshima yao iliyopotea kwa muda mrefu.
        Afisa habari wa klabu hiyo,                Tobias Kifaru Lugalambwika amejitapa na kusema kwamba                maandalizi yanakwenda vizuri na wala hakuna haja ya                kuifananisha na timu ndogo.
        "Mtibwa iko vizuri kweli kweli,                moja ya klabu inayoendeshwa kikampuni, Tunakwenda kwenye                mstari, hatuyumbishwi na watu". Alisema Kifaru.
        Afisa habari huyo aliongeza kuwa                Mtibwa ni klabu bora Tanzania, tofauti na timu changa za                Azam na Mbeya City.
        " Hapa Tanzania klabu bora na                kongwe ni tatu tu, Simba, Yanga na Mtibwa". Alijigamba                Kifaru.
        "Kuna timu zinawika mwaka mmoja                halafu zinatelemka, halafu unaziona tena baada ya miaka 10                au 15. Mtibwa ipo juu na usifananishe ni timu nyingine".
        "Maandalizi ni mazuri na msimu                ujao tutafanya vizuri na kurudi katika hadhi yetu.                Tunakiri kufanya vibaya kwa miaka mingi, lakini sasa                inatosha". Alimaliza Kifaru.
        
Comments
Post a Comment