SIMANZI ZAENDELEA KUTAWALA NDANI YA NYUMBA YA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) MARA BAADA YA MSHIRIKI MWINGINE KUAGA SHINDANO
Majaji                wa shindano la TMT wakimsikiliza kwa makini Mshiriki wa                TMT, Mwanaafa Mwinzago (anayeonekana kwenye runinga mbele)                wakati akijielezea kabla ya filamu fupi aliyoshiriki                kuonyeshwa ili majaji waweze kutoa hukumu kwa washiriki wa                kundi hilo
           Majaji wa Shindano la Tanzania                Movie Talents (TMT) katikati wakiwasikiliza washiriki wa                kundi la kwanza wanavyojielezea kabla ya filamu fupi                waliyochezwa kuonyeshwa katika ukumbi wa Makumbusho ya                Taifa wiki iliyopita
           Majaji wa Shindano la Tanzania                Movie Talents (TMT) wakiangalia filamu fupi iliyochezwa na                washiriki wa shindano la Tanzania Movie Talents (TMT)                katika ukumbi wa makumbusho kabla ya kuanza kutoa hukumu                kwa washiriki ni nani anatoka na nani anabaki.
          Jaji Vyonne Cherry au Monalisa                akitoa maoni kwa washiriki waliokuwa wameshiriki kwenye                filamu fupi iliyochezwa na washiriki wa TMT
            
            Kundi la Kwanza la Washiriki                wa TMT waliocheza filamu fupi iitwayo LUGHA GONGANA wakiwa                mbele ya meza ya Pilato katika ukumbi wa makumbusho ya                Taifa mwanzoni mwa wiki.
           Mshiriki wa TMT, Mwanaafa                Mwinzago akifunika uso wake kwa kutoamini kuwa ameponea                kwenye tundu la sindano kutokana na kuondolewa katika                maumivu ya Jua la Utosi na kuendelea na mashindano hayo
           Mshiriki Wa TMT, Moses Obunde                (Mwenye Suti) akimpongeza Mshiriki Mwenzie Mzee Kapalata                Mtawa kwa kuweza kuondolewa Kwenye Jua la Utosi na                Kupelekwa Kivulini katika Shindano la TMT linaloendelea.
           Washiriki walioingia kwenye Jua                la Utosi wakiwa mbele ya Meza ya Pilato huku mshiriki                mmoja kutoka kwa washiriki hao aliyaaga mashindano ya TMT.
           Simanzi Zikianzia hapo sasa                mara baada ya Washiriki kupunguzwa ili apatikane mmoja wa                kuondoka
           Wakabaki wawili na hatimaye                mmoja kati ya hao aliweza kuondolewa katika mashindano                hayo
           Hatimaye Mshiriki Isalito Isaya                Akaweza kurudi ndani ya Mjengo wa TMT kutokana na Kura                zake kumzidi Mshiriki mwenzie Pendo ambaye aliweza kuaga                mashindano hayo kutokana na kura kuwa chache
          Baadhi ya Washiriki wa TMT                wakimuaga Mshiriki mwenzao Pendo Edward (Katikati) ambaye                aliweza kutolewa kwenye mashindano kutokana na kura kuwa                chache.Picha Zote na Josephat Lukaza
--
          --
Na Josephat Lukaza - Proin                Promotions Limited - Dar Es Salaam.
          Hatua ya mchujo katika Shindano                la Tanzania Movie Talents (TMT) limeingia wiki ya tatu ya                mchujo sasa mara baada ya mshiriki mmoja kuaga shindano                hilo wiki hii. Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT)                limekuwa shindano bora ambalo kadri siku zinavyozidi                kwenda linazidi kuteka nyoyo za watanzania wengi waliopo                ndani na nje ya Nchi kutokana na utofauti wake na uzuri                wake pia.
          
          Mshiriki mmoja ambaye ni Pendo                Edward aliweza  kuchomwa na jua la utosi lililompelekea                kutoka kwenye shindano hilo kubwa la Tanzania Movie                Talents (TMT) ambapo mpaka sasa washiriki kumi na tano                (15) ndio wamebaki katika nyumba ya TMT na hali ya simanzi                bado inaendelea katika nyumba ya TMT kwa wiki hii ambapo                mshiriki mwingine atatakiwa kutoka.
          
          Shindao la TMT limekuwa likivuta                hisia za watanzania wengi waliopo ndani na Nje ya Tanzania                kutokana na Utofauti wake na ubora wake na kupelekea                watanzania wengi sana kufuatilia shindano hilo kwa ukaribu                na umakini zaidi.
          
          Hatimaye wiki hii Tanzania Movie                Talents iliamua kuzindua Zoezi la kuwapigia kura washiriki                wake kupitia ukurasa wetu wa facebook ambapo sasa                watanzania na wapenzi wa TMT ambao wanauwezo wa kupata na                kutumia internet sasa wanaweza kuwapigia kura washiriki                waliowavutia kupitia ukurasa wetu wa facebook na vilevile                kuendelea kuwapigia kura washiriki kwa kutumia simu zao za                mkononi.
          
          Jinsi ya Kumpigia kura Mshiriki                umpendae kwa Kutumia Simu ya Mkononi Andika Neno "TMT" ikifuatiwa na namba ya                ushiriki halafu tuma kwenda 15678.                Mfano TMT 00 tuma kwenda                15678
          
          Na Jinsi ya Kumpigia kura                mshiriki kupitia ukurasa wetu wa facebook BOFYA                    HAPA  kwa kupata maelezo.
        
Comments
Post a Comment