Romelu   Lukaku ameamua kufanya mazoezi na timu yake ya zamani kabla ya kuanza msimu   mpya.MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Romelu Lukaku anajifua na klabu yake ya zamani   ya  Anderlecht kwa lengo la kujiweka fiti kabla ya kuanza msimu mpya wa   ligi kuu soka nchini England.
  Lukaku   bado hajaungana na wachezaji wenzake kutokana na likizo aliyoipata baada ya   kutoka katika fainali za kombe la dunia na timu yake ya Taifa ya   Ubelgiji.
    Mkali   wa mabao: Mshambuliaji wa Ubelgiji, Lukaku  alikuwa katika kiwango cha juu   na klabu yake ya Everton alipokuwa anacheza kwa mkopo msimu   uliopita.
Comments
Post a Comment