PICHA 27 ZA MSONDO NA SIKINDE WALIVYOANGUSHA BURUDANI YA KILO TCC CLUB CHANG’OMBE









PICHA 27 ZA MSONDO NA SIKINDE WALIVYOANGUSHA BURUDANI YA KILO TCC CLUB CHANG'OMBE
PICHA 27 ZA MSONDO NA SIKINDE WALIVYOANGUSHA BURUDANI YA            KILO TCC CLUB CHANG'OMBE

BENDI mbili kongwe kulizo zote zile za dansi, Msondo Ngoma Music Band "Baba ya muziki" na Mlimani Park Orchestra "Sikinde ngoma ya ukae" siku ya Idd Mosi zilionyeshana kazi kwenye viwanja vya TCC Club Chang'ombe.

Lilikuwa ni onyesho la Nani Zaidi ambapo mashabiki ndio waliochiwa waamue wenyewe ipi ni bendi bora zaidi. Hata hivyo, kwa jicho la kawaida ngoma ilikuwa droo.

Lilikuwa ni onyesho zuri la kiutu uzima lililosheheni ufundi wa hali ya juu huku ushabiki mithili ya ule wa Simba na Yanga ukitawala.

Pata picha za onyesho hilo.

 Hassan Rehan Bitchuka akiongoza jahazi la Sikinde
 Shaaban Dede wa Msondo akiimba kwa hisia kali
 Hassan Moshi "TX Junior" moja ya nguzo za Msondo 
 Abdallah Hemba wa Sikinde akishambulia jukwaa
 Jamwaka wa Sikinde katika Tumba
 Joseph Bernad wa Sikinde akipuliza Saxphone
 Waimbaji wa Msondo: Edo Sanga, Shaaban Dede na Juma Katundu

 Juma Katundu (kushoto) na Hassan Moshi (kulia) wakishambulia jukwaa na mashabiki wa Msondo

 Maswahiba! Kichuna wa Kimakua akiwa na Abdulfareed Hussein katika onyesho la Msondo na Sikinde
 Hawa Msondo hawamalizi tu!!? ni kama anahoji mwimbaji wa Sikinde Hassan Kunyata
 Mashabiki wakiselebuka
 Masoud Masoud MC wa mpambano wa Msondo na Sikinde
 Mpiga solo wa Sikinde Adolph Mbinga
 Kazi inaendelea kwa mashabiki wa Msondo na Sikinde
 Wanachama wa kundi la Bongo Dansi (BD) wakifuatilia mpambano
 Meza ya wadau wa Bongo Dansi
 Mwimbaji wa Sikinde Munsemba wa Minyigu 
 Hadi wazungu hawakubaki nyuma
 Mikakati: Ridhwan Pangamawe wa Msondo akipeana mbinu na Shaaban Dede
 Abdul Ridhwan "Panga mawe" wa Msondo akipiga solo gitaa kwa hisia kali
 Roman Mng'ande "Romario" wa Msondo akifanya yake jukwaani
 Shaaban Lendi wa Msondo akipuliza sax
 Shukuru Majaaliwa akiimba kwenye jukwaa la Msondo
 Waimbaji wa Sikinde
 Mwimbaji mpya wa Msondo Twaha Mohamed
 Mashabiki waliojazana mbele ya jukwaa la Sikinde
Sikinde wakishambulia jukwaa



Comments