BENDI mbili kongwe              kulizo zote zile za dansi, Msondo Ngoma Music Band "Baba ya              muziki" na Mlimani Park Orchestra "Sikinde ngoma ya ukae"              siku ya Idd Mosi zilionyeshana kazi kwenye viwanja vya TCC              Club Chang'ombe.
                                                                                   
          Lilikuwa ni onyesho la Nani              Zaidi ambapo mashabiki ndio waliochiwa waamue wenyewe ipi ni              bendi bora zaidi. Hata hivyo, kwa jicho la kawaida ngoma              ilikuwa droo.
          Lilikuwa ni onyesho zuri la              kiutu uzima lililosheheni ufundi wa hali ya juu huku              ushabiki mithili ya ule wa Simba na Yanga ukitawala.
          Pata picha za onyesho hilo.
                     Hassan Rehan Bitchuka            akiongoza jahazi la Sikinde
                     Shaaban Dede wa Msondo akiimba            kwa hisia kali
                     Hassan Moshi "TX Junior" moja            ya nguzo za Msondo 
                     Abdallah Hemba wa Sikinde            akishambulia jukwaa
                     Jamwaka wa Sikinde katika            Tumba
                     Joseph Bernad wa Sikinde            akipuliza Saxphone
                     Waimbaji wa Msondo: Edo Sanga,            Shaaban Dede na Juma Katundu
                     Juma Katundu (kushoto) na Hassan              Moshi (kulia) wakishambulia jukwaa na mashabiki wa Msondo
            
                     Maswahiba! Kichuna wa Kimakua            akiwa na Abdulfareed Hussein katika onyesho la Msondo na            Sikinde
                     Hawa Msondo hawamalizi tu!!?            ni kama anahoji mwimbaji wa Sikinde Hassan Kunyata
                     Mashabiki wakiselebuka
                     Masoud Masoud MC wa mpambano            wa Msondo na Sikinde
                     Mpiga solo wa Sikinde Adolph            Mbinga
                     Kazi inaendelea kwa mashabiki            wa Msondo na Sikinde
                     Wanachama wa kundi la Bongo            Dansi (BD) wakifuatilia mpambano
                     Meza ya wadau wa Bongo Dansi
                     Mwimbaji wa Sikinde Munsemba            wa Minyigu 
                     Hadi wazungu hawakubaki nyuma
                     Mikakati: Ridhwan Pangamawe wa            Msondo akipeana mbinu na Shaaban Dede
                     Abdul Ridhwan "Panga mawe" wa            Msondo akipiga solo gitaa kwa hisia kali
                     Roman Mng'ande "Romario" wa            Msondo akifanya yake jukwaani
                     Shaaban Lendi wa Msondo            akipuliza sax
                     Shukuru Majaaliwa akiimba            kwenye jukwaa la Msondo
                     Waimbaji wa Sikinde
                     Mwimbaji mpya wa Msondo Twaha            Mohamed
                     Mashabiki waliojazana mbele ya            jukwaa la Sikinde
                    Sikinde wakishambulia jukwaa
                                 
Comments
Post a Comment