JUMAMOSI              jioni, mkurugenzi wa kundi la Mashauzi Classic Modern              Taarab, Isha Mashauzi, alifutarisha nyumbani kwake              Hananasif, Kinonondoni jijini Dar es Salaam na kudhuriwa na              watu kibao wakiwemo wasanii wa fani mbali mbali.
                           Ilikuwa ni              tukio moja maridadi sana ambapo watu walipata nafasi ya              kufanya dua, kabla ya kupata ftari na baadae kuwa na wasaa              wa kuongea mawili matatu.
          Kwa              kuzingatia kuwa Mashauzi Classic hawatakuwepo jijini Dar es              Salaam katika msimu wote wa sikukuu ya Eid el Fitr, ftari              ile ikawa ni wasaa mzuri wa kutakiana kheri za sikukuu              ambayo inatarajiwa kuanza Jumatatu au Jumanne kutegemea na              mwandamo wa mwezi.
          Pata picha              kibao za tukio hilo
                     Watoto wa Madrasa wakipata            ftari
                    Hapa ilikuwa ni wasaa wa kupata            dua
                    Dua inaendelea
                    Masupastaa wa movie za kibongo            Gabo (kushoto) na Yussuf Mlela
                    Gabo akikaribishwa na meneja wa            Mashauzi Classic, Ismail "Suma Raga" (kulia)
                    Kutoka kushoto: Gabo, Suma            Raga, Kassim Mganga, Hashim Said
                    Mtoto wa Isha Mashauzi            Ibtidaiyaht 
                    Mpiga kinanda wa Mashauzi            Kalikiti Moto (kushoto) akiwa na fundi mitambo wao
                     Msanii wa bongo fleva Kassim            Mganga (kushoto) akihojiwa na TBC
                    Asha Manga (kushoto) na msanii            wa bongo fleva Shetta wakipata ftari ya upendeleo baada ya            kuchelewa kufika
                    Watu wa kila namna walihudhuria
                    Mwigizaji Hemed PHD akipata            ftari
                     Mtangazaji wa East Africa            Radio Mwanne Othman akisaidaia kukarangiza mapocho pocho
                    Baadhi ya waalikwa
                    Waimbaji wa zamani wa Jahazi            Modern Taarab Isha Mashauzi (kushoto) na Mwanne Othman
                     Sehemu ya umati uliofurika            nyumbani kwa Isha Mashauzi
                    Hemed na Isha katika picha ya            pamoja baada ya ftari
                    Mama mzazi wa Isha Mashauzi Bi            Rukia Juma
                     Saluti5 ikipata wasaa wa            kufanya mahojiano na TBC
                     Shetta na mwimbaji wa Mashauzi            Classic Hashim Said
                    Watu walikuwa ni wengi sana            kiasi kwamba nyumba ilionekana ndogo
           
                                 
Comments
Post a Comment