PICHA 10 ZA SHOW YA TWANGA PEPETA MANGO GARDEN …wasanii wapya watambulishwa, Diouf atoweka, Asha Baraka atoa kauli




PICHA 10 ZA SHOW YA TWANGA PEPETA MANGO GARDEN …wasanii wapya watambulishwa, Diouf atoweka, Asha Baraka atoa kauli
PICHA 10 ZA SHOW YA TWANGA PEPETA MANGO GARDEN …wasanii            wapya watambulishwa, Diouf atoweka, Asha Baraka atoa kauli

ONYESHO la Twanga Pepeta siku ya Idd Mosi pale Mango Garden, lilikuwa moja ya maonyesho bab kubwa yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Twanga Pepeta walipiga show ya nguvu, wakatambulisha madansa wanne wapya kutoka Extra Bongo: Sabrina, Maria, Danger Boy na Hamza Mapande.

Hata hivyo watu wengi waliofika kwenye onyesho hilo, hawakufanikiwa kumuona rapa Msafiri Diouf kama ilivyokuwa imeelezwa hapo awali kuwa msanii huyo naye anarudishwa kundini na atatambulishwa siku ya Idd Mosi.

Hakukuwa na sababu zozote zilizotolewa ukumbini hapo juu ya kukosekana kwa Msafiri Diouf na hivyo kuwafanya washabiki wengi wabaki njia panda.

Hata hivyo, baadae Saluti5 iliongea na mkurugenzi wa Aset Asha Baraka ambaye alikuwa na haya ya kusema kuhusu rapa huyo:

"Diouf ameomba atambulishwe rasmi Jumamosi Mango Garden kwa vile anataka ashuke na vitu vipya.

"Ameshiriki mazoezi kwa siku 2, tulitarajia tumtambulishe siku ya Idd Mosi lakini tumeamua kumfanyia tukio maalum Jumamosi ijayo ili ajinoe zaidi." Alimaliza Asha Baraka. 

 Kulia kabisa dansa aliyerejea Twanga, Maria Soloma
Dogo Rama
Hajj BSS
Dansa mwingine aliyerejea Twanga, Sabrina
 Kalala Jr akiwa na Amos wa Mashujaa Band aliyekwenda kusalimia jukwaa la Twanga
 Rapa na mwimbaji J Four akishambulia jukwaa
Mpiga solo Miraji Shakashia
Danger Boy  aliyerejea Twanga kutoka Extra Bongo
Mashambulizi kwa kwenda mbele
Dansa mpya kutoka Extra Bongo, Hamza Mapande "Dogo White"

 

 



Comments