OZIL, MERTESACKER, PODOLSKI HATARINI KUKOSA MECHI YA UFUNGUZI LIGI KUU ENGLAND

 
 
 
 
Arsene Wenger poses for a picture with New York Red Bulls star Thierry Henry (second left)
Arsene Wenger akipozi katika picha na nyota wa  New York Red Bulls, Thierry Henry (wa pili kushoto).
KOCHA wa Asernal, Mfaransa,  Arsene Wenger ameweka wazi kuwa wachezaji wake watatu walioshinda kombe la dunia wana uwezekano mkubwa wa kukosa mechi ya ufunguzi ya ligi kuu soka nchini England dhidi ya Crystal Palace.
Mesut Ozil, Per Mertesacker na Lukas Podolski wapo likizo mpaka Agosti 11 mwaka huu baada ya kuisaidia Ujerumani kutwaa kombe la dunia nchini Brazil.
Nyota hao watarudi London zikisalia siku tano tu kabla ya kuanza ligi dhidi ya kikosi cha Tony Pulis.
The Arsenal players train in the New York Red Bulls stadium ahead of Saturday's match
Wachezaji wa Asernal wakifanya mazoezi kwenye uwanja wa  New York Red Bulls kuelekea mechi ya kirafiki kesho jumamosi.
Arsene Wenger chats to former Gunners hero Thierry Henry who now plays for the New York Red Bulls
Arsene Wenger akizungumza na shujaa wa zamani wa washika bunduki Thierry Henry ambaye kwasasa anaichezea New York Red Bulls

Wenger wachezaji wake watatu washindi wa kombe la dunia wanaelekea kukosa mechi ya kwanza ya msimu.
Mfaransa huyo alisema: "Nimewapa likizo nzuri kwasababu nina uzoefu na wachezaji waliokuwa katika fainali ya kombe la dunia. Unahitaji kupumzika".
"Watakuwa tayari?  Mertesacker anajiandaa vizuri - lakini kwa mchezo wa kwanza Agosti 16 sidhani kama watakuwa tayari".
Wenger aliyekataa kuthibitisha kama amemuadhibu Jack Wilshere baada ya kupigwa picha akivuta sigara, pia aliwaibukia FIFA na kuwaambia wanatakiwa kufirikia upya ratiba yao kwasababu imempa ugumu katika kikosi chake.
A fit again Abou Diaby tussled for the ball during the session in New York
Abou Diaby akijiweka fiti kwenye mazoezi mjini New York.

Comments