Kocha wa Mwadui fc,                Jamhuri Kiwhelo 'Julio'
        Na Baraka Mpenja, Dar                es salaam
        TIMU ya Mwadui                fc ya Shinyanga inatarajia kuanza mazoezi ya kujiandaa na                msimu mpya wa ligi daraja la kwanza unaotarajia kuanza                mwezi Octoba mwaka huu.Kocha mkuu wa klabu hiyo, Jamhuri                Musa Kiwhelu 'Julio' amesema mazoezi hayo yataanza katika                viwanja vya Leaders Club jijini Dar es salaam ambapo                baadhi ya wachezaji wa Mwadui watahudhuria.
        "Tunaanza mazoezi kesho                katika viwanja vya Leaders kwa baadhi ya wachezaji wa                Mwadui kuhudhuria.Tunatarajia kuwa na timu bora yenye                ushindani mkubwa, kwahiyo Kesho saa kumi jioni tunaanza                mazoezi," Alisema Julio.
        Julio aliongeza kuwa                klabu yake inahitaji kufanya usajili wa wachezaji wengine                kwasababu muda unakimbia sana.
        Kocha huyo alibainisha                kuwa wameamua kuitisha majaribio ya wachezaji, hivyo kwa                wote wanaojiona wana vipaji wafike kesho Leaders.
        "Wachezaji walioachwa                Simba, Yanga wafike kujaribiwa. Tunawakaribisha watu wote                wenye uwezo," Alisema Julio.
        
Comments
Post a Comment