KOCHA wa Chelsea, Jose   Mourinho amethibitisha kuwa mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo, Didier Drogba   anarudi darajani.
  Nyota huyo raia Ivory Coast  aliitumikia Chelsea   kwa miaka 8 na kuondoka mwaka 2012  ambapo alijiunga  Galatasaray   ya  Uturuki baada ya kutwaa kombe la UEFA dhidi ya Bayern Munich.
  Ingawa ana miaka 36   kwasasa, Mourinho anaamini bado anaweza wa kucheza ligi kuu nchini England na   michuano ya kimataifa.
  "Tunalifikiria hilo," Mreno   huyo aliwaambia waandishi wa habari baada ya kuulizwa uwezekano wa Drogba   kurudi.
  "Tunahitaji kushinda mechi   na kushinda makombe na Didier ni moja ya washambuliaji bora barani   Ulaya,".
  "Bado anao uwezo wa kucheza   ligi kuu na tunalifikiria sana hilo na hatuendeshwi kwa   hisia".
"Kama unamrudisha, si   kwasababu yeye ni Didier au alifunga magoli mengi muhimu katika historia yake   Chelsea, au kwasababu nahitaji msaidizi, hapana, namrudisha na maamuzi yamekuja   mapema kwasbaabu yeye kama mchezaji anaweza kuifanya timu kuwa   imara".
Comments
Post a Comment