NA FULLSHANGWE
        MAISHA ya soka ya Mido                yameingia ukurasa mwingine baada ya kufukuzwa kazi ya                ukocha mkuu na klabu yake ya Zamalek jana jumanne.
        Kocha huyo kijana                mwenye miaka 31 aliripotiwa kuwa na mgogoro na bodi ya                klabu na kusababisha kibarua chake kuota nyasi, japokuwa                inasemekana kuwa ataendelea kuwa sehemu ya miamba hiyo kwa                majukumu mengine.
        Mido alirithi mikoba ya                Helmy Toulan mwezi januari mwaka huu na aliiongoza timu                hiyo kucheza mechi za mwisho za ligi ya ndani na kutwaa                ubingwa wa kombe la Misri mbele ya klabu ya Smouha.
        Licha ya kupata                mafanikio hayo, Mido aliyekaa kwa miezi saba tu                aliripotiwa kuwa na matatizo mengi na bodi ya klabu hiyo,                lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Zamalek atapewa                majukumu mengine klabuni hapo.
        Mido alisema: "Ahmed                Suliman kutoka bodi ya ukurugenzi ameniambia maamuzi yao                ya kunifukuza".
        "Bado ni mtoto wa                Zamalek na niko tayari kufanya kazi yoyote kuisaidia                klabu".
        Mido alistaafu kucheza                soka akiwa na miaka 30 mwezio juni mwaka 2013, huku akiwa                amezichezea klabu 12 tofauti, zikiwemo Zamalek, Ajax,                Marseille, Roma na Tottenham, kabla ya kuichezea Barnsley                alipotundika daruga zake.
        
Comments
Post a Comment