MASHUJAA BAND KUIZUNGUKA TANZANIA NZIMA …kutia mguu hadi KENYA …uhondo unaanzia Mtwara Idd Mosi …Bavaria yatoa udhamini

 
 
 
 
MASHUJAA BAND KUIZUNGUKA TANZANIA NZIMA …kutia mguu hadi KENYA …uhondo unaanzia Mtwara Idd Mosi …Bavaria yatoa udhamini

BENDI bora ya dansi kwa mwa mwaka wa pili mfululizo, Mashujaa Band inatarajia kufanya ziara kubwa ya kuzunguka karibu mikoa yote ya Tanzania, hii ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya bendi hiyo.

Ziara hiyo itakayochukua zaidi ya wiki mbili, ambayo itahusika hadi maonyesho kadhaa nchini Kenya, inakuja kufuatia maombi mengi ya mashabiki wa mikoani lakini pia ni pamoja na kutoa shukran kwa wapenzi wao kila sehemu walioiwezesha Mashujaa Band kutwaa tuzo tatu za Kilimanjaro Tanzania Music Awards.

Kwa mujibu wa ratiba ambayo Saluti5 imetumiwa na Mkurugenzi Masoko wa Mashujaa, Max Luhanga, ni kwamba ziara hiyo itaanzia Mtwara siku ya Idd Mosi katika ukumbi wa Makonde Beach huku Idd Pili wakiwa Masasi katika ukumbi wa kisasa wa Emirates.

Katika hali ya kuvutia zaidi, Saluti5 imeambiwa kuwa zaidi ya nusu ya show hizo tayari zimenunuliwa na mapromota wa mikoani hali inayoonyesha ni namna gani watu wana hamasa na ziara hiyo ya Mashujaa Band.

Kinywaji cha Bavaria kimedhamini ziara hiyo ya Mashujaa na tayari magari mawili (mini bus na gari la vyombo) yameshapigwa chata za kuvutia kunadai tripu hiyo. Mwishoni mwa habari hii utapata picha 6 za magari hayo.

Ratiba kamili ya ziara hiyo ya Mashujaa Band ni kama ifuatavyo.

IDD MOSI: MAKONDE BEACH- MTWARA.

IDD PILI: EMIRATE HALL- MASASI

30-07-2014  NACHINGWEA-
NACHINGWEA RESORT

31-07-2014  MBINGA-MBINGA RESORT

01-08 2014  SONGEA-SERENGETI PUB

02-08-2014  MBEYA-CITY PUB

03-08-2014  MBALALI TOP LIFE

05-08-2014  TUNDUMA-HIGH CLASS

06-08-2014  SUMBAWANGA-MWAMBAO PUB

07-08-2014  MPANDA- KATAVI RESORT

08-08-2014  KIGOMA-SANDRA NIGHT CLUB

09-08-2014  TABORA- BWALO LA MAOFISA WA POLISI.

10-08-2014  SHINYANGA-NSSF HALL

13-08-2014  KAHAMA- CLUB CHILLER

14-08-2014  BUKOBA- LINAS CLUB

15-08-2014  GEITA-DESIRE CLUB

16-08-2014  MWANZA-VILLA PARK

17-08-2014 MWANZA-BUZURUGA

20-08-2014 MUSOMA MAGEREZA HALL

21-08-2013--KENYA
22-08-2014--KENYA
23-08-2014--KENYA
24-08-2014--KENYA

28-08-2014  KOROGWE MAMBA CLUB

29-08-2014  TANGA - NYUMBANI HOTEL

30-08-2014  ARUSHA -  TRIPPLE A

31-08-2014  SINGIDA - LAKE GARDEN

05-09-2014  DODOMA- CANIVALL

06-09-2014  Dar...Kill Award Event.

07-09-2014 MOROGORO-NYUMBANI PARK.

Max Luhanga amesema maonyesho mengine ya mikoani yanaweza kuongezeka kadri ya mahitaji ya mapromota wa sehemu husika.

Pichani ni namna magari ya Mashujaa Band yalivyoandaliwa kwa ziara hiyo.

Bus la wanamuziki linavyoonekana kwa ubavuni
Gari la kubebea vyombo linavyoonekana kwa nyuma
Gari la kubebea vyombo linavyoonekana kwa ubavuni
  Bus la wanamuziki linavyoonekana kwa mbele
  Gari la kubebea vyombo linavyoonekana kwa mbele
Bus la wanamuziki linavyoonekana kwa nyuma

Comments