IVORY COAST KUTAJA KOCHA MPYA, HERVE RENARD APIGIWA CHAPUO `BAB KUBWA`



IVORY COAST KUTAJA KOCHA MPYA, HERVE RENARD APIGIWA CHAPUO `BAB KUBWA`
CHANZO MPEJA 
IVORY Coast itatangaza jina la kocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo kesho alhamisi mchana, kwa mujibu wa shirikisho la soka.
Shirikisho lilisema kwamba, usaili wa mwisho kwa majina  matatu yaliyosalia unakamilika leo jumatano mjini Abidjaan, mji mkuu wa nchi hiyo na mji mkuu wa kibiashara.Mfaransa Herve Renard anaonekana kuwa ndiye atashinda nafasi hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vya mtandao wa michezo wa Supersport.com ndani ya shirikisho la nchi hiyo.
Beki huyo wa zamani mwenye miaka 45, aliyeiongoza Zambia kutwaa ubingwa wa kombe la mataifa ya Afrika, AFCON 2012, anafurahia kuungwa mkono na viongozi wakubwa wa soka na wizara ya michezo ya Ivory Coast.
Hata hivyo, kocha wa zamani wa Sporting na Benfica, Jose Manuel De Jesus kutoka Ureno naye anaonekana kupewa nafasi ya juu kutokana na uzoefu wake mkubwa kwa soka la ulaya. Lakini hajawahi kuongoza timu ya taifa, kitendo ambacho vyanzo vinaeleza kuwa kitamuangusha katika nafasi hiyo.
Herve Renard anapewa nafasi kubwa ya kuwa kocha mpya wa Ivory Coast

Mfaransa mwingine, Frederic Antonetti, aliyeifundisha Rennes, pia anapewa nafasi miongoni mwa majina matatu ya mwisho yaliyotolewa wiki iliyopita na shirikisho la soka. Ingawa hana uzoefu wa kufundisha timu ya taifa, lakini ujuzi wake wa kuendeleza vipaji unampa nafasi ya kuchaguliwa.
Zaidi ya makocha 37 waliomba kazi hiyo, akiwemo kocha wa zamani wa Tembo hao, Francois Zahoui. Katika orodha hiyo, majina yalipunguzwa mpaka matano na baada ya usaili wa pili yakabakia matatu ambayo yanasailiwa kwa mara ya mwisho.

Kocha mpya atapewa kazi ya kuiandaa timu kwa ajili ya kufuzu kucheza michuano ya Afrika mwaka 2015 nchini Morocco.


Comments