GUARDIOLA: TULIJITAHIDI KUMSHAWISHI TONI KROOS ABAKI BAYERN

 
 
 
 
Guardiola: We tried to convince Kroos to stay
BOSI wa Bayern Munich, Pep Guardiol amesema walijitahidi kufanya kila kitu kumshawishi Toni Kroos asaini mkataba mpya Allianz Arena.
Nyota huyo mwenye miaka 24 alijiunga na Real Madrid mwezi huu baada ya mazungumzo na Bayern juu ya mkataba mpya kuvunjika mapema mwaka huu.
Guardiola alikiri kuwa mabingwa hao wa Bundesliga walimshawishi mshindi huyo wa kombe la dunia kuendelea kubakia klabuni na kushindikana, lakini Bayern imemtakia maisha mema katika maisha yake mapya ya soka.
"Tulijitajiihi kumshawishi abakie klabuni, lakini naelewa. Ni kijana na anataka changamoto mpya. Ni maamuzi yake na tumeyaheshimu," aliwaambia waandishi wa habari.

"Natumaini ana furaha Madrid. Ilikuwa heshima kuwa kocha wake. Namtakia kila la kheri yeye na familia yake. Wakati huo huo napenda kumshukuru kwa yale aliyofanya msimu uliopita".

Comments