
Mshambuliaji wa Ivory Coast              Didier Drogba amesaini mkataba wa mwaka mmoja kujiunga tena              na Chelsea.
                  Drogba,                36, alishinda makombe 10 akiwa na Chelsea kuanzia mwaka                2004 hadi 2012, na alikuwa mchezaji huru baada ya kuondoka                klabu ya Galatasaray ya Uturuki.
                      
Meneja                  Jose Mourinho, mapema alisema Stamford Bridge ni kama                  "kwake" mchezaji huyo.
                          Drogba ameiambia tovuti ya Chelsea kuwa:                  "Ulikuwa uamuzi rahisi- sikuweza kukataa nafasi ya                  kufanya kazi tena na Jose."
            
Comments
Post a Comment