ATLETICO MADRID SASA YAMTAKA CHICHARITO WA MAN UNITED


ATLETICO MADRID SASA YAMTAKA CHICHARITO WA MAN UNITED

Last chance saloon: Javier Hernandez could be                  shipped out of Old Trafford if he does not impress his                  new boss

KOCHA wa Atletico Madrid, Diego Simeone ameweka wazi kuwa angependa kupata saini ya mshambuliajia wa Mexico na Manchester United "Chicharito".

Hernandez amekuwa akihusishwa na kutimka United  dirisha hili la usajili kufuatia msimu mbovu aliokuwa nao Old Trafford.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alianza mechi sita tu za Ligi Kuu msimu uliopita akiachwa nyuma na washambulijiaji Robin van Persie, Wayne Rooney na Danny Welbeck.

Simeone amesema Hernandez ni mchezaji wa hali ya juu na anayeweza kuwa muhimu kwenye timu yoyote ile.

"Tunazungumza na wakurugenzi wa michezo na kuwaeleza aina ya mchezaji tunayemtaka na baada ya hapo ni juu yao kumsajili.

"Kukiwa na Javier Hernandez pamoja na wachezaji wengine wazuri, lolote linawezekana. Hatufungi mlango hadi dirisha la usajili litakapofungwa.



Comments