Na                  Othman Khamis Ame, OMPR
        Timu ya Soka ya African                Boys ya Kijiji cha Kitope imetawazwa ubingwa wa mashindao                ya Kombe la Zaweda baada ya kuitandika timu ya New Star ya                Kiwengwa kwa Magoli 4 -3 katika pambano la fainal ya                mashindano hayo yaliyoshirikisha Timu 12 za Soka za Jimbo                la Kitope. 
        African Boys ya Kitope                ilibeba kombe hilo la Zaweda baada ya kutoka suluhu ya                bila kwa bila na wapinzani wake New Star ya kiwengwa                kwenye dakika 90 za mchezo huo na kulazimika kupigiana                Penalti zilizoibua mshindi wa pambano hilo lililofanyika                katika uwanja wa michezo wa Santiago Benabao uliopo                Kitope. 
        Mgeni rasmi wa Fainali                hiyo Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili                wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikabidhi zawadi                kwa mshindi wa kwanza African Boys ya Kitope ambayo                ilipata fedha taslim shilingi Laki 500,000/-, Seti ya                Jezi, Kikombe, Mipira pamoja na Seti ya Tv na Dikoda yake                iliyotolewa na Mke wa Mbunge wa Jimbo hilo Mama Asha                Suleiman Iddi.
         Mshindi wa Pili New                Star ya Kiwengwa ikazawadiwa shilingi Laki 300,000/-                taslim, Jezi, Kikombe pamoja na Mipira wakati mshindi wa                tatu Timu iliyoalikwa ya soka ya Mahonda Kids                akajinyakulia shilingi Laki 200,000/- Taslim, jezi pamoja                na mpira. Mapema Balozi Seif alikabidhi zawadi ya fedha                taslim kwa washindi wa mashindano ya mchezo wa pete {                netball } ambapo mshindi wa kwanza ni timu ya wanawake ya                Biasha Kitope, mshindi wa Pili alikuwa timu mualikwa                Mahonda na wa Tatu alikuwa Timu ya Mabanati wa Kitope " B                ". 
        Akizungumza na wana                michezo hao wa mashindano ya Zaweda Cup Mbunge wa Jimbo la                Kitope Balozi Seif alielezea furaha yake kutokana na zoezi                zima la mashindano hayo lililoonyesha nidhamu ya hali ya                juu na kuwataka wanamichezo hao kuhakikisha kwamba nidhamu                hiyo wanaichukulia kuwa kigezo cha kuiendeleza katika                michezo mengine itakayowakabili hapo baadaye. 
                 Mbunge wa Kitope                  Balozi Seif ali Iddi akizungumza na wanamichezo mara                  baada ya kumalizika kwa fainali ya mashindano ya Zaweda                  Cup hapo uwanja wa michezo wa Kitope Wilaya ya Kaskazini                  " B". Kushoto                  yake ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini " B "                  Ndugu Hilika Khamis Fadhil.
                 Balozi Seif                  akikabidhi zawadi za mipira na jezi kwa timu shiriki za                  mashindano ya Zaweda Cup yaliyofanyika ndani ya Jimbo                  lake la  Kitope.
                 Balozi Seif                  akikabidhi zawadi za mipira na jezi kwa timu shiriki za                  mashindano ya Zaweda Cup yaliyofanyika ndani ya Jimbo                  lake la  Kitope.
                 Balozi Seif                  akikabidhi zawadi za mipira na jezi kwa timu shiriki za                  mashindano ya Zaweda Cup yaliyofanyika ndani ya Jimbo                  lake la  Kitope.
                 Mabingwa wapya wa                  kombe la Zaweda African Boys ya Kitope wakishangilia                  ushindi wao dhidi ya New Star ya Kiwengwa kwa mikwaju ya                  Penalti 4-3 baada ya kumaliza muda wa dakika 90 bila kwa                  bila.
                Wanandinga                    wa African Boys ya Kitope wakiitia mikononi seti ya TV                    aina ya Phillips na King'amuzi chake ikiwa ni miongoni                    mwa mzawadi walizojikusanyia baada ya kushinda fainali                    ya kombe la Zaweda dhidi ya New Star ya Kiwengwa. Picha na                    Hassan Issa wa  OMPR
        





Comments
Post a Comment