PICHA 22: UZINDUZI WA ALBAM MPYA YA MASHAUZI CLASSIC BALAA! MANGO GARDEN YATAPIKA …Isha naye aacha gumzo



PICHA 22: UZINDUZI WA ALBAM MPYA YA MASHAUZI CLASSIC BALAA! MANGO GARDEN YATAPIKA …Isha naye aacha gumzo
PICHA 22: UZINDUZI WA ALBAM MPYA YA MASHAUZI CLASSIC            BALAA! MANGO GARDEN YATAPIKA …Isha naye aacha gumzo

UZINDUZI wa albam mpya ya Mashauzi Classic "Asiyekujua Hakuthamini" uliofanyika Alhamisi usiku, umefana, umesisimua, umekosha, umefurahisha na kuacha gumzo la aina yake.

Ukumbi wa Mango Garden Kinondoni ambao ndio uliokuwa nyumba ya uzinduzi huo, ulijaa hadi kutapika huku burudani zote kuanzia zile za usindikizaji hadi uzinduzi wenyewe, zikiwapagawisha vilivyo mashabiki waliofurika ukumbini hapo.

Mkongwe Ally Star, Cassim Mganga na Ben Pol walifanya vema katika kusindikiza uzinduzi wa "Asiyekujua Hakuthamini" lakini mandhari ya ukumbi wa Mango Garden ikabadilika kabisa majira ya saa 6 za usiku pale mkurugenzi wa Mashauzi Classic, Isha Ramadhan alipoingia jukwaani kwa staili ya aina yake. (Katika habari itakayofuata baada yah ii, tutakusimulia namna Isha alivyoingia sambamba na mtiririko mzuri wa picha zitakazokupa sura kamili ya tukio hilo).

Kwa hakika lilikuwa ni onyesho bab kubwa na ilikuwa ni zawadi nzuri ya kufunga msimu wa kwanza wa burudani mwaka 2014 (kabla ya kuanza mfungo wa Ramadhan) – Hakukuwa na dosari yoyote hata kama ungeitafuta kwa tochi bado usingeiona – Mashauzi walijipanga vizuri.

Albam ya ASIYEKUJUA HAKUTHAMINI inaundwa na nyimbo tano: "Asiyekujua Hakuthamini" ulioimbwa na Isha na mdogo wake (Saida Ramadhan), "Bonge la Bwana" wa Hashim Said, "Ni Mapenzi tu" wa Zubeda Malick, "Ropokeni yanayowahusu" uimbaji wake Saida Ramdhan na "Wema Hauozi na Ubaya haulipizwi"  wa Asia Mzinga.

Ally Star akipagawisha  
Cassim Mganga naye akisindikiza onyesho la Mashauzi
Ben Pol pia alikuwepo
Ben Pol akikonga nyoyo za mashabiki
Isha na madansa wake katika mwendo wa kiasili
Hapo sasa
Hapa Isha akiimba na mdogo wake Saida Ramadhan
Saida Ramadhan huyo
Mtu na dadake
Mkongwe Mwanamtama Amir akiselebuka na goma la Mashauzi
Unaweza kujionea nyomi iliyokuwepo ukumbini
Mtu na mama yake: mwimbaji Asia Mzinga akitunzwa na mama yake mzazi Bi Mwanamtama Amir
Hashim Said akiimba wimbo "Bonge la Bwana" 
Hashim akipewa mshiko na mdau anayefahamika kama Poti Poti
Isha akiimba wimbo "Mapenzi hayana dhamana"
Burudani inaendelea
Saida Ramadhan akitunwa mshiko na mumwe
Watangazaji Dida wa Times FM (kushoto) na Mwanne Othman wa East Africa Radio
Hapa ni wimbo "Ropokeni yanayowahusu" kutoka kwa Saida Ramadhan
 Dida akiongea machache jukwaani
Bi Rukia Ramadhan na Ally Star

 



Comments