Mcheza soka wa                          timu ya taifa ya Ghana, Sulley Muntari, ni                          maarufu sana kwa umahiri wake anapokuwa dimbani                          kama alivyo maarufu katika simulizi tamu za                          ukarimu, upendo na kuwahurumia watu. Wakati                          michuano ya Kombe la Dunia ikiendelea Muntari                          ameonekana peke yake akizunguka katika mitaa ya                          Rio de Janeiro na kuwapa pesa watu maskini                          wanaoishi jirani na e
neo ambalo timu yake                            inafanyia mazoezi katika jiji hilo.
                            
                            Michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu wa 2014                            imeathiriwa na visa vya ubaguzi, mashabiki                            wakaidi na ukosefu wa usawa, lakini kiungo                            huyo wa Ghana Sulley Muntari anatengeneza                            vichwa vya habari tofauti kabisa kwa matendo                            haya ya wema na utu.
                            
                            Mapema Alhamisi, siku mbili kabla ya mchezo                            ambao timu yake ilitoka sare ya 2-2 dhidi ya                            Ujerumani, Muntari aliomba ruhusa kutoka kwa                            Kocha wake Kwesi Appiah kwenda kutembea katika                            mitaa ya Trapiche (jirani na mji wa Maceio,                            ambapo timu yake imeweka makazi) na kuanza                            kutoa fedha kuwapa watu maskini katika eneo                            hilo. Ripoti moja inasema kuwa alikuwa akitoa                            kiasi cha R$350 (fedha ya Brazil), ambayo ni                            sawa na kiasi cha $160 kwa kila maskini                            aliyekutana nae.
                            
                            Hatimaye polisi wa eneo hilo walimtaka aache                            kufanya hivyo.
                            
                            "Siwezi kulisahau tukio hili," bwana Edivaldo                            aliyebahatika kupata msaada huo aliuambia                            mtandao wa Globo.com.
                            "Nimeishi katika jamii hii maskini nyuma ya                            uwanja wa soka wa Rei Pele kwa miaka arobaini                            lakini sikuwahi kuona kitu kama hiki. Hakuna                            hata siku moja mwanasoka alikuja hapa. Brazil                            haikunipa chochote lakini Muntari wa Ghana                            amenipa. Niwaunga mkono na kuwashangilia mpaka                            mwisho."
                            "Mimi na mama yangu mwenye umri wa miaka 80                            tumepata R$350 [fedha za Brazil]," anasema                            Inês Corrêa, aliyekuwepo katika tukio hilo                            baada ya polisi wa eneo hilo kumzunguka                            Muntari. "Ninaamini alikuwa na R$5,000 lakini                            kwa bahati mbaya polisi walimzuia kufanya                            tendo hili jema. Katika eneo hili tunawaona                            wanasiasa pekee tena wakati wa uchaguzi."
                            
                            Je, unajua kuwa wakati wa biashara ya Utumwa                            Waafrika zaidi ya milioni thelathini                            walipelekwa Brazil kupitia Bahari ya Atlantic                            katika matukio yanayojulikana kama Maafa? Ni                            dhahiri kuwa Muntari anajua kuwa wale wenye                            nyuso nyeusi nchini Brazil ni wenzetu.                            Zitazame mwenyewe nyuso za watu wa Brazil,                            kama wewe ni Mwafrika popote utakapokuwa hapa                            duniani basi wewe ni sehemu ya familia hii                            moja.
                            
                            Suleyman Ali "Sulley" Muntari, aliyezaliwa                            Agosti 27 mwaka 1984, ni mcheza soka raia wa                            Ghana ambaye anacheza nafasi ya kiungo wa kati                            katika Klabu ya Milan ya Italia. Akiwa katika                            klabu yake ya Internazionale, aliisaidia                            kutwaa ubingwa wa Klabu Bingwa barani Ulaya                            kwa msimu wa mwaka 2009–10 na Ubingwa wa ligi                            ya nchini humo maarufu kama Serie A kwa mwaka                            2008–09 na 2009–10. Pia alikuwa katika kikosi                            cha Portsmouth kilichoutwaa Kombe la chama cha                            Soka cha Uingereza, FA, kwa mwaka 2007–08. Ni                            kaka mkubwa wa mchezaji wa CFR Cluj Sulley                            Muniru.
Comments
Post a Comment