Matumaini ya bara la Afrika            kuingiza timu kwenye hatua ya 16 bora ya michuano ya kombe la            dunia yameanza kupotea.Wakicheza mchezo wao muhimu na wa            mwisho, Ivory Coast ilikubali kipigo kutoka kwa Ugiriki katika            mchezo ulioisha kwa kufungwa 2-1.Kufuatia ushindi huo Ugiriki            imeungana na Colombia kwenda hatua ya pili kutoka kwenye kundi            hilo.Ugiriki ilikuwa ya kwanza kufunga kupitia bao la kwanza            la Georgios Samaras kunako dakika ya 42 ya kipindi cha kwanza            baada ya mlinzi wa Ivory Coast Cheick Tiote kufanya makosa ya            kipuuzi.
        Ivory Coast hata hivyo              ilifunga bao la kusawazisha kupitia Wilfried Bony aliyetumia              vyema pasi safi kutoka kwa Gervinho.
        Ugiriki walipata goli la              kupitia penati ya dakika za majeruhi iliyofungwa na Samaras              tena.
        Colombia ilikamilisha              mechi za makundi kwa kuiadhibu Japan 4-1 na kuweka rekodi ya              kushinda mechi zote katika makundi.
        
Comments
Post a Comment