Michuano ya Kagasheki Cup 2014                imeendelea tena leo kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba Mjini                kwa siku ya pili na kushuhudia mahasimu wawili Mmoja                akimliza mwenzake bao 3-0.
        Mtanange wa leo hii Jumapili                ulizikutanisha timu mbili matata kwenye hii ligi za Kashai                na Bakoba FC na kushuhudia Timu ya Bakoba ikifungwa bao                3-0 bao zilizofungwa kipindi cha kwanza mbili na kipindi                cha pili moja.
        Timu ya Kashai FC                  walianza kuifunga timu ya Bakoba bao la kwanza katika                  dakika ya 8 bao likifungwa na Joha Johansen. 
          Bao la pili lilifungwa                  na Msengi Gerard katika dakika ya 38 kipindi cha kwanza                  na kufanya bao kuwa 2-0 dhidi ya mahasimu wao Bakoba                  ambao mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika walikuwa                  hawajapata kitu.
          Kipindi cha pili licha                  ya timu zote mbili kukamiana kwa sana timu ya Bakoba                  ilipata nafasi kama tatu lakini haikuweza kuifunga timu                  ya Kashai na hatimaye Kashai kupata bao lao la tatu                  katika dakika ya 60 kipindi cha pili bao lililotiwa                  nyavuni na Mchezaji wa Kashai FC Shamte Odilo na Kipute                  kumalizika kwa dakika 90 Kashai ikiibuka kwa bao 3-0. 
          Michuano hii                  itaendelea tena kesho Jumatatu na kutakuwa na Mitanange                  miwili wakwanza utachezwa saa nane kati ya Nshambya FC                  ikiumana na timu ya Kibeta Fc saa 8:00 mchana na                  mtanange wa saa 10:00 ni baina ya Kagondo Fc na Buhembe                  Fc.
        Dakika 90 zimemalizika waamuzi wanatoka uwanjani                  ...
          Kashai 3 vs Bakoba 0.
                  
Comments
Post a Comment