Jazz Band 2 (Rashid Hanzuruni)



Western Jazz Band 2 (Rashid Hanzuruni)

Rashid Hanzuruni, kama ilivyo watu wote walio mahiri katika vyombo vyao vya muziki alilipenda gitaa lake na alifanya mazoezi kila alipopata muda. Kwa maelezo ya mtu aliyekuwa karibu nae alisema huyu bwana kuna wakati dansi likisha isha watu wanaenda kulala yeye aliwasha tena mashine na kuanza mazoezi ya gitaa. Kuna hadithi ambayo hata mimi niliiamini kwa miaka mingi kuwa Doctor Nico alipokuja Tanzania alimuulizia Hanzuruni, hadithi hii si ya kweli. Kwa malezo ya mtu aliyekuweko kipindi hicho, Western Jazz walialikwa kupiga pamoja na Dr Nico alipokuja Tanzania kati ya mwaka 66 na 67, na katika maonyesho hayo, kwanza Hanzuruni ndipo alipomuona Dr Nico kwa karibu na kupenda staili ya upigaji wake, na pia ndipo alipomuona Dr Nico akipiga Hawaian Guitar, nae akalipenda na Western Jazz wakalinunua na Hanzuruni akawa mpigaji wa kwanza Mtanzania wa gitaa la hawaian,baada ya hapo Hanzuruni alifanya sana mazoezi ili aweze kupiga gitaa kama Dr Nico. Ni vizuri kulisema hapa kuwa Hanzuruni ndie alikuwa mwanamuziki aliyelipwa vizuri kuliko mwanamuziki yoyote wa Dar Es Salaam wa aina yake, katika kipindi hicho.



Comments