Wamenaswa: Mashabiki                  wawili waliojipaka rangi nyeusi wakiwa katika pozi                  kwenye mchezo baina ya Ujerumani na Ghana.
            SHIRIKISHO la soka                  Duniani, FIFA linachunguza picha zilizozagaa                  zikiwaonesha mashabiki wakiwa wamejipaka rangi nyeusi                  katika mchezo wa kundi G baina ya Ujerumani na Ghana.
            Picha zilizochapishwa                  kwenye mitandao ya kijamii zinaonesha wanaume wawili,                  wanaoonekana kuwa mashabiki wa Ujerumani, wakiwa na sura                  nyeusi kwenye uwanja wa Fortaleza jumamosi iliyopita.
            FIFA imesema kamati                  yake ya maadili ipo katika majadiliano ya kufungua kesi.
          Wanatazama mechi:                  Mashabiki wawili walinaswa na kamera katika sare ya 2-2                  baina ya Ujerumani dhidi ya Ghana.
            "Siku zote tunachukua                  ushahidi wote na kuupeleka kamati ya maadili. Ni kamati                  ya maadili itakayokutana," Msemaji wa FIFA amewaambia                  The Guardian. "Kama kutaonekana kuna ukweli kesi                  itafunguliwa. Hilo lipo juu ya kamati ya maadili, wao                  ndio watachukua maamuzi".
            FIFA huwa                  wanayawajibisha mashirikisho ambayo mashabiki wake                  wanaonesha utovu wa nidhamu uwanjani.
            Katika tukio la pili,                  mtu aliingia uwanjani kipindi cha pili wakati wa sare ya                  2-2.
            Mtu huyo ambaye hakuwa                  na shati aliripotiwa kuwa ni Mpoland na alijiandika                  namba za simu na anwani ya barua pepe tumboni kwake.
            Kiungo wa zamani wa                  Portsmouth na Sunderland, Sully Muntari, ambaye kwasasa                  anacheza AC Milan alimsalimia mtu huyo kabla ya                  kuondolewa na maaskari wa usalama.
            Msemaji wa kamati ya                  maandilizi ya Brazil, Saint-Clair Milesi alisema mtu                  huyo aliingia kutokana na uzembe wa mamlaka zinazohusika                  na usalama uwanjani.
          
Comments
Post a Comment